Thursday, April 28, 2011

WAZIRI WA KAZI NA AJIRA MHE.GAUDENSIA KABAKA AHUTUBIA SONGEA LEO

 Waziri wa Kazi na Ajira Mhe.Gaudensia kabaka akihutubia maelfu ya wafanyakazi katika uwanja wa majimaji  Katika Manispaa ya Songea leo katika kilele cha maadhimisho ya 8 ya usalama na afya kazini
 Waziri katika  picha ya pamoja na baadhi ya wafanya kazi





Waziri na vikombe kabl haja kabidhi kwa washindi  hapo chini.
W
 Waziri akimkabidhi kikombe cha ushindi wa jumla Bw.Isack Senya

Ajali kazini husababisha hasara na kupunguza uzalishaji – Kabaka

KILA mwaka serikali imekuwa ikipoteza wafanyakazi wake kwa kupoteza maisha au sehemu za viungo vyao vya mwili katika sehemu zao za kazi pengine bila ya kuwa na taarifa kutoka kwa wa waajiri,vyama vya wafanyakazi kwa kutokuwa na takwimu za watu walioathirika  mahali pa kazi.

Waziri wa kazi na Ajira  Mhe. Gaudensia Kabaka alisema hayo siku ya maadhimisho ya 8 ya usalama na afya kazini yaliyo fanyika kitaifa Mjini Songea katika uwanja wa majimaji leo.

Mhe.Kabaka alisema Serikali,waajiri na wafanya kazi pamoja na vyama vya wafanyakazi  lazima kuzingatia kanuni zilizo wekwa na Shirika la Kazi Duniani ( ILO ) la kuwa na sheria zitakazofuatwa. Za usalama na afya kazini.

Alisema ukiona watu hawaendi kazini kila mara ujuwe sehemu hiyo si salama,hivyo kuwe na kanuni na sheria zitakazo fuatwa na kila mfanya kazi na kuwa na vifaa vya kujikinga na ajali hasa sehemu za ujenzi,migodi na kwenye viwanda.ili kupunguza ajali.

Baada ya kufunga maadhimisho hayo Mhe.Kabaka aligawa zawadi kwenye makampuni tisa ambayo yameonyesha umahili wao katika usalama na afya kazini ,zawadi hizo likuwemo vikombe pamoja na vyeti.

No comments:

Post a Comment