Saturday, April 30, 2011

ILO YAIPONGEZA SERIKALI YA TANZANIA KWA KURDHIA BIKATABA YA USALAMA NA AFYA KAZINI

Mwakilishi wa Shirika la Kazi Duniani Bwana Magnus Minja akisoma hotuba ya Bwana Alexio Musindo,Mkurugenzi wa ILO Ofisi ya Tanznaia,Kenya ,Uganda na Rwanda  wakati wa maadhimisho ya usalama na afya kazini tarehe 28 mwezi huu Songea Mkoa wa Ruvuma


SHIRIKA la kazi Duniani ( ILO ) laipongeza serikali ya Tanzania kwa kuwa tayari na sheria ya usalama na afya kazini mwaka 2003 ambapo mikakati inaendelea ya uhakiki wa utekelezaji wake.

Mwakilishi wa Shirika la kazi Duniani Bwana magnus Minja alisema hayo kwenye kilele cha maadhimisho ya usalama na afya kazini kilichofanyika mkoani Ruvuma tarehe 28 mwezi huu.

Bw.Magnus alisema kuwa Tanzania imekwisharidhia baadhi ya mikataba inayohusiana na usalama na afya kazini ambayo ni mikataba Na..148 wa mwaka 1977 unaohusu mazingira ya kazi,Na.152 wa mwaka 1979 unaohusu usalama na afya kazini,kazi za bandarini na ule wa  Na.170 wa mwaka 1990 unaohusu matumizi ya kemikali.

Alisema ni matarajio ya Shirika hilo kuwa juhudi za serikali na wadau wengine wataendelea kuchukua jitihada zaidi ili kuridhia mikataba mingine iliyobakia ukiwemo mkataba Na.187 wa mwaka 2006.Pamoja kuwepo kwa masharti ya usalama kazini hasa kwenye makampuni makubwa,pia kuyasaidia makampuni madogo katika utekelezaji wake kwa vitendo.

No comments:

Post a Comment