Thursday, February 14, 2013

MKUU WA MKOA WA RUVUMA SAID THABITI MWAMBUNGU AMETOA SIKU 14 KWA WAZAZI NA WALEZI AMBAO WATOTO WAO HAWAJA RIPOTI SEKONDARI KIDATO CHA KWANZA , BAADA YA ZIARA YA KUSHITUKIZA KATIKA SHULE 5 KWA KILA WILAYA

 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw.Said Thabiti Mwambungu akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake leo.
 Mkuu wa Wilaya Songea Bw.Joseph Joseph Mkirikiti
 Afisa Elimu Mkoa ( REO ) Ruvuma.
Baadhi ya waandishi wa habari.wakimsikiliza mkuu wa mkoa.



MKUU wa mkoa wa Ruvuma Bw.Said Thabiti Mwambungu ametoa siku kumi na nne kwa wazazi na walezi ambo hawaja wapeleka shule za sekondari watoto wao ambao wamechaguliwa kuingia kidato cha kwanza mwaka huu.
Mkuu huyo wa mkoa amesema hayo katika ofisi yake leo alipokuwa akiongea na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari kuhusu tatizo hilo la watoto wengi ambao wamechaguliwa kuingia kidato cha kwanza mkoani humo lakini hadi tarehe 14/2/2013 hawaja pelekwa shule.
Ameagiza wakuu wa wilaya,wakurugenzi,mkatibu tarafa ,na watendaji  wa vijiji na mitaa ambao wanaishi wa wazazi na walezi wa watoto hao kuwahimiza kuwapeleke shule kabla ya tarehe 01/03/2013 kwa hiyari yao, na kwamba baada ya tarehe hiyo kupita wazazi na walezi watachukuliwa hatua kali za kisheria.
Aidha Bw.Mwambungu amesema tatizo hapa sio ada bali ni miundombinu ya wazazi na walezi wa watoto hao kuwa mibaya.Kwa kuwa ada ya  shule ni shilingi 20,000 kwa mwaka,muhula wa kwanza shilingi 10,000 na muhula wa pili shilingi elfu kumi.
Aidha alisema kuwa idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza mkoani humo mwaka huu ni 16,578 lakini walioripoti ni 9,388 tu, na wanafunzi 7,190 hawajaripoti katika shule za sekondari walizopangiwa.

No comments:

Post a Comment