Monday, February 18, 2013

HIVYO WENYE HAKI YA KUISHI NI VIONGOZI WA DINI YA KIISLAMU PEKE YAO , TANZANIA ?, TANGU MAUAJI HAYO YAANZE NCHINI UMEWAHI KUSIKIA KIONGOZI WA DINI YA KIISLAMU KAUAWA NA WAKRISTO ? TATIZO LIKO WAPI ?

Hayati Padre Evaristus Mushi,jana kafikia mikononi mwa Ibilisi wakati akienda kusoma misa ya Ibada takatifu huko Unguja,Tukioa la kwanza ni kuchoma makanisa hakuna aliyeshtuka,lakini hatukusikia misikiti imechomwa moto,la pili Padre kavamiwa na kujeruhiwa hili nalo halikuchukuliwa mkazo,utadhani ni paka alikoswakoswa kuuawa,sasa funga kazi ni lajana la kumpiga risasi na kumuua padre wa watu.

Wakati Kamanda PC Mussa Ali Mussa wa Zanzibar anadai watu kadhaa wamekamatwa kwa mauaji hayo,ila hajui ni akina nani wanahusika na wimbi la mauaji na vurugu katika Kisiwa hicho,wala wa kuwatuhumu hawa jui na wala hawezi kusema ni sababu ya kisiasa au kudini, Hapo suala la kisiasa halipo kwa asilimia kubwa taka usitake,lakini yote kwa Mungu.

Ja Serikali ya Baraza la Mapinduzi Zanzibar imetamka nini kuhusu hilo? , unadhani ni jambo la kawaida hilo ? ,je Kuna siri gani imejificha katika Fasihi hii ?. Kumbe tukiona mbwa amekenua meno tusidhani kuwa amefurahi, anaweza akatung'ata ?.kumbe ni kweli wakati wa biashara ya watumwa uhai wa mtu ulikuwa mikononi mwa mtu mwingine mwenye uwezo na siyo Mungu aliyetuumba?.E Mungu uwasamehe watu hao hawajui walilolitenda kwa Marehemu Mushi,na ilaze roho yake mahali pema peponi Amina.


SUALA  la mauaji wa viongozi wa Dini ya madhehebu ya Kikristo yanaendelea, na hakuna hata siku imetokea wauaji wamekamatwa, ila Serikali inasisitiza tu kuwa  walaifu wasakwe na wakamatwe mara moja basi muda utapita hakuna kinacho endelea.

Swali linakuja,hivyo tangu mauaji hayo yametokea ni lini umesikia kiongozi wa Madhehebu ya Kiislamu kauawa au amepigwa? Au ni lini umesikia misikiti imechomwa moto zaidi ya Makanisa ? Kama msomaji, hujapata kusikia vipi hili limetokea na linazidi kutokea serikali halilioni hilo, utadhani wanaofanyiwa hivyo ni wanyama wasiyo na thamani ya kuishi katika nchi hii ambayo  inaitwa kisiwa cha Amani,amani imetoweka,ni kazi kweli kuirudisha kwa mtindo huu unaoendelea

Hivyo Tanzania wanaotakiwa kuishi kwa amani ni waislamu peke yao ? .Ingawa wauaji hao sina uhakika kuwa ni wa kutoka dhehebu gani ,lakini yamkini ni kutoka katika Dhehebu hilo.

Tunaianzisha Tanzania ya matabaka ya udini ambayo Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliyapiga vita vikali.Tunahangaika na kitu gani,kila mtu anaimani yake ambayo anafikiri akiifuata hiyo itampeleka peponi,isitoshe wote tuna mwabudu Mungu mmoja ingawa kila taifa lina jina lake wanalomwita Mungu wao.

Mitume wote  waliyo tumwa na Mungu kuja kuwakomboa wanadamu kutoka dhambini binadamu wa karne hii tunawaumini tu, wala hatuwahi kuonana nao wala siyo kutoka katika makabila yetu bali ni imani tu ya kuwaamini,lakini sisi kwa sisi ambao wote hawaja kutana nao uso kwa uso tunauana, niushabiki usiyo na maana wala busara,kwani hakuna mwenye haki ya kucheza na uhai wa mwenzake, kazi hiyo tumwachie Mungu.

Hivyo basi  serikali yetu sikivu iliangalie kwa macho ya karibu matukio hayo, watu wa madhehebu ya kikristo wanaishi kwa mashaka, kwani nchi hii inatawaliwa na serikali ya kidini?,kama serikali inaweza kutenga maeneo ya wakulima na wafugani ,kwanini sasa wasitenge maeneo ya madhehebu Fulani peke yao ili wasichanganyike nao kuwe  na amani katika kuabudu kwao.Haipendezi inasikitisha sana tunachoka kusikia historia hiyo hiyo kila wakati. ( Padre Evaistitus  Mushi ) maskini alikuwa akienda kuendesha ibada, matokeo yake kafikia mikononi kwa Ibilisi. Poleni Familia ya Padre Mushi.





No comments:

Post a Comment