Tuesday, February 26, 2013

KISIWA CHA AMANI TANZANIA SASA KINATAKA KUWA KISIWA CHA BALAA SOMA UJUMBE HUO UNAOSAMBAZWA KWENYE SIMU ZA WATU JE KAMA NI KWELI WAKRISTO WAIHAME NCHI YAO ?, NA SERIKALI INAPATA UJUMBE MBALIMBALI UNAOTISHIA UHAI WA WATANZANIA?

NANUKUU Ujumbe huo,'Tahadhali kundi la waislamu toka Dar, Tayali limeshawasili mikoani  kwa ajili ya kuja kubomoa na kuchoma makanisa, tunatakiwa makini tuwapo makanisani hata katika kazi zetu, usipuuzie ni taarifa kutoka Jimbo kuu la Dar es Salaam. Wajulishe Mapadri,Watawa na makatekista, Wachungaji, Wainjilisti, Mapastor na wakristo wote, ni vema na haki kusambaza ujumbe huu kwa kasi zaidi na kuwajulisha wakristo wote, upatapo ujumbe huu tuma kwa waombaji 12.
   Na si ujumbe huu tu bali kuna mahubiri katika baadhi ya Miskiti ambayo yanatishia amani kwa wakristo na CD zipo zinaonyesha kwa kiasi gani Madhebu ya Kikristo yanavyo pigwa vita na kutishia amani katika uhai wao, Je Serikali inalifahamu hilo,kama lina fahamu ni hatua zipi zinachukuliwa ili kunusuru uhai wa wakristo nchini?.
  Mbona matokeo mabaya ya kidato cha nne tunasikia Tume imeundwa kutoka Zanzibar kuna wajumbe watatu ( 3 ) ?, nini zaidi kutishiwa kwa uhai wa watu au Kufeli kwa wanafunzi?, Inasikitisha  sana huwa tunasikia tu Mashariki ya Kati sasa tunaona Live Emungu tutaukumbuka maneno ya Baba wa Taifa kama  kuna ukweli wowote kwa watu wanaosambaza ujumbe huo.
 Na kama hakuna ukweli kwanini waendelee kusambaza na serikali inawafumbia macho wasambazaji?

1 comment:

  1. Panapotokea janga, kama lile la kuchomwa moto na kuibiwa mali ya makanisa kule Mbagala, serikali inakuwa mstari wa mbele kwenda kuwapa pole waathirika, badala ya kuwadhibiti wanaoleta hizo fujo ili wasifurukute kabisa.

    ReplyDelete