Thursday, February 14, 2013

BAADHI YA WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI WAMEKANUSHA KUWEPO KWA BURE. KITU AMBACHO SI CHA KWELI.

 Wakuu wa shule za sekondari za Mashujaa na Mazoezi Matogoro wakileza jinsi wanafunzi wa kidato cha kwanza wanavyo ripoti kwa kusua sua hadi sasa.Mwenye kaunda suti nyeusi kushoto ni Bw.Leonard Matao wa Shule ya sekondari Mashujaa na wa kulia mwenye shati nyekundu ni Mkuu wa shule Mazoezi Matogoro Bw. Marianusi A. Komba.
 Bw.Marianus A,Komba
Bw.Leonard Matao

 

BAADHI ya wakuu wa shule za sekondari katika Manispaa ya Songea wamekanusha  kuwepo kwa utitili wa michango katika shule zao za sekondari.wamesema kuwa michango ambayo inachangishwa ni michango ambayo inasaidia kuendesha shule.
Wamesema kuwa Serikali haipeleki fedha ambazo zingilipwa kwa kila mtoto kusaidia wazazi na walezi kama walivyopanga,hivyo kamati ya shule na wazazi na walezi wanakubaliana kuchangisha fedha ili kuziba mapengo ambayo serikali ilipaswa kuchangia kwa kila mtoto kama ilivyo ahidi.
Kuhusu watoto kutoripoti shule wale waliyochaguliwa kuingia kidato cha kwanza , Mkuu wa shule  ya sekondari Mazoezi Matogoro Bw.Marianus A. Komba na Mkuu wa shule Mashujaa Bw.Leonard Matao wanasema ni kweli kwamba bado kuripoti kwa wanafunzi waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza hakuridhishi.
Hivyo wakuu hao wanaungana na tamko la Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kuwa wazazi na walezi kuwapeleke watoto wao shule kabla ya tarehe 01/03/2013 aliyo sema mkuu wa mkoa huyo,

No comments:

Post a Comment