Friday, September 16, 2011

SEMINA YA SIKU MBILI YA WAANDISHI WA HABARI INAENDELE JIJINI MBEYA

Semina hiyo inahusu maadili ya waandishi wa habari inayoendeshwa kwa vyama vya waandishi wa habari katika mikoa nchini.( Press clubs}.tunawatakia mafunzo mema ,pia wayashike mafundisho wanayo elekezwa na walimu wao.kila kazi ina maadili,miiko yake ili ifanyike katika utaratibu uliyowekwa.

Hivyo waandishi ndiyo kisemeo katika jamii,waandishi ndiyo wanaowasemea wasio na sauti katika jamii,kwa maantiki hiyo hawatakiwi kuipotosha jamii kwa kutumia kalamu zao,au kuichonganisha jamii kwa uwezo waliyokuwa nao.Pia wanahaki ya kupata habari na kuiandika.
Pamoja na hayo na wadau wa habari nao wana nafasi yao ya kutoa habari hata kama inaumiza kwake lakini itanufaisha taifa.Hivyo mtoa na mpokea habari wote wana nafasi kubwa kwa jamii.

No comments:

Post a Comment