Tuesday, November 30, 2010

IKIWA LEO NI MAADHIMISHO YA UKIMWI DUNIANI LAKINI UKIMWI BADO NI TATIZO KATIKA JAMII ZETU,KILA MMOJA WETU ACHUKUE TAHADHARI - MNJAGILA

Mkurugenzi wa Elimu ya Watu Wazima na Nje ya Mfumo Rasmii Bwana Salum Mnjagila akitia saini kitabu cha wageni katika ofisi ya Afisa Elimu Wa Halmashauri ya Songea Vijijini Mkoani Ruvuma mwaka huu wakati wa ziara ya kukagua vituo vya MUKEJA na VICOBA  Simanjiro,Njombe,Songea,Na Mahenge.( picha na Christian Sikapundwa )

Bwana Mnjagila pamoja na kukagua maendeleo ya vituo hivyo lakini hakusita kutoa tahadhari yuu ya VVU na UKIMWI katika jamii za watanzania.Alisema wanapojifunza jinsi ya kuzalisha mali katika ufugaji,ususi biashara ndogondogo na uwekaji wa akiba benki ,lakini pia wajifunze namna ya kuacha mambo yanayochangia maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kwa kuwa na mpenzi mmoja,kauacha mambo hayo au kutumia kinga.Hata kusikiliza ushauri wa wataalamu wa afya na ushauri wa viongozi wa Dini.

No comments:

Post a Comment