Sunday, November 28, 2010

Siku 16 za kupinga ukatili za kijinsia Tanzania,wanaharakati,jamii isilifumie macho jambo hilo

Siku 16 za maandalizi ya kupinga ukatili wa kijinsia miongoni mwa watanzani,unafanyika kikanda kama ilivyo ainishwa na wanaharakati wa kupinga unyanyasaji wa kijinsia katika jamii zetu za kitanzania.Hasa kufuatia mila na desturi za kiafrika kuwa na mfumo dume,mfumo boss,na hata mfumo jike.Dkt Judith Tudunga alisema kupitia vyombo vya habari kuwa ukatili wa kijinsia umetawala sana katika jamii zetu.

Wito wake kwa watanzania kuwa wakisikia jirani anapigwa ama kufanyiwa vitendo ambavyo vinamdharirisha wajitokeze kwenda kutoa msaada.Alisema unyanyasaji na ukatili wanaofanyiwa baadhi ya tanzania unasaidia kurudisha nyuma maendeleo ya ,mtu binafsi na hata Taifa zima kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment