Friday, November 5, 2010

DOKTA JAKAYA KIKWETE ATANGAZWA KUWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BAADA YA KUPATA ASILIMIA 61.17

Dokta Jakaya Kikwete atangazwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kushinda kwa asilimia 61.17,akifuatiwa na Dokta Willbroad Slaa wa CHADEMA kwa asilimia 26.34 na hakufika kwenye matangazo hayo,ambapo mshidi wa tatu ni Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF aliyepata asilimia 8,06.

Profesa Lipumba alimpongeza Dokta Kikwete kwa ushindi aliyoupata na kumpatia Ilani ya CUF isaidie kuleta Demokrasia nchini,katika ahadi kadhaa zilizo ahidiwa wakati wa kuwaomba wanachi ridhaa ya kuiongoza nchi.kama vile ajila kwa vijana,kuboresha elimu,miundombinu na ustawi wa jamii.

Dkt Kikwete kawashukuru watanzania wote kwa kuichagua CCM,Tume ya Uchaguzi,Vyombo vya habari kwa mchango wao,Wangalizi wa Uchaguzi,na kuwaeleza wananchi kuwa uchaguzi umepita kwa utulivu na Amani.

No comments:

Post a Comment