Tuesday, November 30, 2010

wakati leo ni maadhimisho ya UKIMWI Duniani Ruvuma wapo chini ya 33% ya upimaji wa hiyari


KAIMU Mratibu wa UKIMWI Mkoani Ruvuma Dkt Luitrid Komba asema changa moto bado ni kubwa kwa watu kujitokeza kupima afya zao kwa hiyari mkoani Ruvuma.Atoa wito kuwa watu wakapime afya zao,dawa za kurefusha maisha zinapatikana katika vituo vinavyo husika.

Wakati leo ni siku ya maazimisho ya UKIMWI Duniani mkoa wa Ruvuma ina asilimia 6.3 kutokana na taarifa ya watu waliojitokeza kupima afya zao Januari hadi Septemba mwaka huu.

Kaimu Mratibu wa UKIMWI mkoa wa Ruvuma Dkt.Luitfrid Komba alitoa taarifa hizo kwenye kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa RCC kilichofanyika Songea Club Novemba mwaka huu.

Dkt Komba alisema upimaji wa hiyari UKIMWI ni asilimia chini ya asilimia 33 kimkoa na kiwango cha watoto walioambukizwa ni asilimia 4.6.Aidha vituo 90 vinatoa huduma ya mama na mtoto ya kinga ya maambukizi ya UKIMWI.
 

No comments:

Post a Comment