Saturday, November 6, 2010

DOKTA JAKAYA MRISHO KIKWETE AMEAPISHWA LEO KUWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO KWA KIPINDI CHA MIAKA MITANO IJAYO

Baada ya kuapishwa Rais na Makamu wa Rais waliombewa Duwa na madhehebu ya kidini ili kuwaombea waongoze kwa amani na utulivu.Kisha alikaribishwa kuwahutubia wananchi alisema hawezi kusema mengi,mengi atasema siku ya kuhutubua Bunge siku chache zijazo.

Ametoa shukurani kwa Mungu,na wananchi kuchagua CCM kwa kuona jinsi walivyo jiandaa kulitumikia taifa.Alisema watembeeni kifua mbele kwani watanazia bado wanaipenda CCM,pia alimshukuru Makamu wa Rais na mke wake kwa kumsaidia katika kufanikisha azima ya kuwa Rais.

Aidha alisema hakuweza kusahau viongozi wa vyama vya siasa vilivyotoa hamasa kubwa kwa CCM,Alisema uchaguzi umepita sasa watu wagange yajayo.Katika baadhi ya maeneo kulipandikizwa sumu mbaya ya kuwagawa watanzania  aliomba yaachwe hayo.


Alisema  watanzania wasiaharibu sifa ya Tanzania ya amani na utulivu kwa lengo la kupata madaraka.pia aliwapongeza Tume ya Uchaguzi jinsi ilivyo fanikisha uchaguzi huu uluyopita,vyombo vya usalama na vyombo vya habari .

No comments:

Post a Comment