Friday, November 12, 2010

SPIKA WA KWANZA MWANAMKE WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE.ANNE SHEMAMBA MAKINDA WA CCM ALIYE PATA KURA 265 SAWA NA ASILIMIA 74.2 AMEANZA KAZI YA KUAPISHA WA BUNGE MARA BAADA YA KUTANGAZWA KWAKE MJINI DODOMA LEO TAREHE 12/11/2010

 Mheshimiwa Samwel John Sitta  Spika aliyestaafu akimkimbatia Mhe. Anne Shemamba Makinda Spika wa CCM  aliyechaguliwa na wabunge hao kwa kupata kura 265. sawa na asilimia 74.2 na kumshinda Mgombea wa  nafasi hiyo Bwana Mabere Nyauchi Marando wa CHADEMA  kwa kura 53 sawa na asilimia 16.2.Baada ya Mhe.Sitta kuaapa kuwa atahifadhi,atailinda na kuitetea katiba ya Jamhuri ya Tanzania iliyowekwa..
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungaqno wa Tanzania aliyechaguliwa kushika nafasi hiyo Mhe. Anne Shemamba Makinda akipeana mikono na Mhe.John Momose Cheyo baada ya kuapa kuwa atakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Rashid Ally Abdalah akipeana mikono na Spika wa Bunge la 10 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Anne Shemamba Makinda baada ya kuchaguliwa kuwa Spika wa Bunge hilo na kuahidi kuwa ataendesha Bunge hilo kwa kanuni za Bunge zilizo wekwa kwa mujibu  bila upendeleo.

No comments:

Post a Comment