Tuesday, November 16, 2010

WAZIRI MKUU MIZENGO KAYANZA PETER PINDA ATHIBITISHWA KWA KURA 277 SAWA NA ASILIMIA 84.5 ZILIZOPIGWA NA WABUNGE WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda mbunge wa Jimbo la katavi amethibitishwa  kwa Waziri Mkuu kwa kupigiwa kura na wabunge 328,ambapo kura zilizoharibika ni 2 sawa na asilimia 0.6,waliosema hapana 49 sawa na asilimia 4.9 na waliosema ndio ni 277 sawa na asilimia 84.5

Baada ya kuthibitishwa kwake Mhe.Pinga alimshukuru Mungu ,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,wahehsimiwa Wabunge kwa kuthibitisha kuwa Waziri Mkuu,aidha alisema kuwa atakuwa Waziri mkuu wa wabunge wote,waliomkataa na waliomkubali kwa lengo la kumsaidia mwananchi.

Alisema kuwa kweli yeye ni mtoto wa mkulima hivyo ameomba ushirikiano mkubwa na wabunge wote wakulenga mkulima,mfugaji,mvuvi na mrina asali,hata kukiwa na malumbano lakini yawe yana lenga  kumtetea mwananchi mkulima.


No comments:

Post a Comment