Monday, November 29, 2010

PONGEZI

Mwenye kiti wa Ruvuma Press Bwana Juma Nyumayo kulia aliyevaa vuti akiwa na Makamu wake wa Press hiyo Bwana Mhidini Ndolanga aliyevaatai na Mjumbe wa Press hiyo Bi.Editha Karlo  wa katikati akiwa akipata chai siku ya kikao cha kamati ya Maendeleo ya mkoa wa Ruvuma hivi karibuni Songea Club ( Picha Na Christian Sikapundwa )


Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Ruvuma (RPC) kinawapongeza viongozi waliochaguliwa  wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Kilimanjaro ( MECK ) kwa kuaminika na wanachama wao na kuwapa ofisi yao ambayo ni mdau mkubwa wa maendeleo.

Mwenyekiti wa Ruvuma press club Bwana Juma Nyumayo,amesema kamati ya muda chini ya uongozi wa mwenyekiti Josephine Sanga,ilifanya kazi nzuri na kuweka misingi imara kufikia uchaguzi wa Kidemokrasia uliowachagua viongozi wapya.

Hongera sana endeleeni kushirikiana kwa maendeleo ya Kilimanjaro,Kanda ya Kaskazini na Taifa zima kwa ujumla ( Source Juma Nyumayo ).

No comments:

Post a Comment