Saturday, December 4, 2010

RUVUMA YA FAULISHA KWA ASILIMIA 47.98 NA KUSHUKA KWA ASILIMIA 8.02 YA MWAKA JANA

Mshauri wa Elimu Mkoa wa Ruvuma Bibi Paulina Mkonongo akisoma taarifa ya maendeleo ya Elimu katika kikao cha Ushauri RCC katika ukumbi wa Songea Club hivi karibuni.


MKOA wa Ruvuma imefaulisha kwa asilimia 47.98,ya wanafunzi watakaoingia kidato cha kwanza mwaka huu,ikiwa imeshuka kwa asilimia 8.02 kwa matokeo ya mtihani wa taifa uliyofanyika  mwaka 2009.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mshauri wa Elimu wa Mkoa wa Ruvuma Bibi Paulina Mkonongo,mbele ya Kaimu katibu Tawala wa Mkoa huo,alisema  wanafunzi 30,829 mkiwemo wavulana 14,986 na wasichana 15,843 waliofanya mtihani huo mwaka huu,kati yao 14,792 mkiwemo wavulana 7,537 na wasichana 7,255 ndio walio faulu sawa na asilimia 47.98. Ambao wataingia kidato cha kwanza mwakani.

Aidha alisema kuwa waliochaguliwa bweni ni wanafunzi ni 103,ambapo wenye vipaji ni 31 wavulana 17 na wasichana 14,wanaokwenda ufundi ni 30 wavulana 27 na wasichana 3.Na waliochaguliwa kutwa  ni 14,689 wavulana 7,469 na wasichana 7,220.

No comments:

Post a Comment