Friday, April 26, 2013

MIAKA 49 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR RAIS KIKWETE KATOA MSAMAHA WA WAFUNGWA 4,180

 Rais Kikwete akimaliza kukagua gwaride katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam katika sherehe za Miaka 49 wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,Uliyo anzishwa na Waasisi Baba wa Taifa na Aman Abed Karume
Picha ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
 Picha ya Rais wa Zanzibar Karume zilizo yumika na watoto wa halaiki wakati wakiimba wimbo maalumu.
 Halaiki walitengeneza maumbo mbalimbali yenye mafundisho.Umbo la kwanza lilikuwa miaka 49 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
 Kikosi cha bendera kilitoa heshima mbele ya Jukwaa kuu.
 Rais akielekea Jukwaani baada ya kukagua gwaride.
 Kama unavyona Herufi hizo
 Maumbo mbalimbali
Umbo hilo ni mazao ya biashara,Ninawapongeza waliofanya kazi hiyo ya kufundisha vijana hao ,wakawa mahili katika kutengeneza maumbo hayo kwa kutumia miili yao na mavazi yao.Nawapongeza sana,lakini cha ajabu bado kuna watu wanaobeza kazi za mwalimu,wanamacho lakini hawaoni wanaimani lakini hawa amini kazi za walimu.Kazi hiyo isingefanikiwa bila ya mwalimu kuingia hapo.Hata kama si mwalimu aliyofanikisha Halaiki hiyo,basi kafanya kazi ya mtu anaitwa mwalimu, japo hakupata Methodology.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, ametoa msamaha kwa wafungwa 4,180 ,ili waende kuungana na familia zao,na kwamba watakuwa wamepata fundisho na wataishi vyema kwenye jamii walizotoka.
Aidha msamaha huo haukuwausu waenye kifungo cha maisha, watumiaji madawa ya kulevya.
 
Maadhimisho ya miaka 49 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilijumuisha Gwaride lilokuwa na Guard 10.ambazo zilikaguliwa na Rais. Na ndege za mafunzo za kivita zilionyesha umahili uliyotumika na marubani wa ndege hizo,ambapo ndege ya tano iliendeshwa na Luteni Kanali Sinzia.
Pia kukawa na watoto wa halaiki 2,695 wa kutoka Tanzania Bara na Tanzania Visiwani ambao walinyesha mazoezi ya viungo,kutengeneza maumbo mbalimbali yenye mafundisho.Na wazheza sarakasi 35 ambao walionyesha michezo kadhaa matika kustarehesha wananchi waliyofurika uwanja wa Uhuru.
Sherehe hizo zilipambwa na ngoma kutoka Tarime Mkoa wa Mara,Gonga kutoka Mkoa wa Kusini Pemba na Sindimba kutoka Mkoa wa Lindi na kwaya kutoka JKT  Masange  Tabora.

No comments:

Post a Comment