Sunday, March 31, 2013

TANZANIA HAINA HISTORIA YA UMWAGAJI WA DAMU KWA RAIA WAKE HATA WAKATI WA KUDAI UHURU WAKE , ILA SASA TUNAONA DALILI ZA UMWAGAJI WA DAMU KWA BAADHI YA RAIA WAKE.

 Askofu Mkuu Dkt Norbert Mtega akibariki waumini baada ya Ibada ya PASAKA Kanisa kuu la Songea leo.
Waumini wakiwa katika Ibada ya PASAKA
 Waumini
 Kwaya ya DONBOSCO ambayo imekoleza ibada hiyo leo siku ya PASAKA
 Zifuatazo ni picha za umoja wa Wanamama Katoliki ( WAWATA) ,Wa Jimbo la Songea
 Kutoa vipaji akina mama ( WAWATA)

 Vipaji akina mama ( WAWATA )
Katika masomo ya Ibada ya PASAKA akina mama wa WAWATA wakipeleka Biblia ili kwenda kusoma na baadaye Injili.Aliyeshika Biblia menye gauni la kijani ni Bi. Cosensa Mbena na wa pili ni Bi Geni.

KATIKA Ibada ya PASAKA kwenye kanisa kuu la  Katholiki la Jimbo kuu la Songea la Mt.Mathias Mulumba Kalemba mjini Songea,ambao waumini wa kanisa hilo waliungana na wenzao Duniani kote kwa sherehe za PASAKA,
Hata hivyo alisema kuwa nchi ya Tanzania haikuwa na Historia ya umwagaji wa damu hata wakati wa kudai Uhuru wake,lakini kuna baadhi ya raia wamemwaga damu kutoka kwa watu wasio eleweka.
Hayo yametolewa katika mahubiri ya Askofu Mkuu wa Jimbo hilo,Dkt.Norbert Mtega katika Ibada ya sherehe za PASAKA leo,na kwamba ukombozi wa Yesu Kristu kwa kufa na kufufuka kwake uwe kwa watu wote wanao mwamini Mungu hata kama hawajabatizwa.
Aliwashukuru sana waandishi wa habari katika mchango wao wa kuandika na kuripoti uharibifu na vifo kadhaa vilivyo jitokeza katika nchi yetu na wengine  kupata vilema vya kudumu kama vile kutolewa macho.
Alisema kuwa waumini waende kumtangaza ufufuko wake wa  amani,upendo na mshikamano,bila ya kujali tofauti za Imani miongoni mwao,kwani wote ni wana wa Mungu.
Aidha alisema kuwa waumini wanatakiwa kuwa na Biblia mikononi mwao,nyumbani kwao na msalaba ambao ni ukombozi wao,kwani Biblia ni neon la Mungu la uzima ,nasio kama vitabu vingine.na kwamba wanawake wameonekana kuwa na mwamko wa kuwa na Biblia na kushiriki katika Jumuia ndogondogo.

Amewataka wanaume nao kushiriki katika uinjilishaji kwa kwenda kwenye Jumuiya ndogondogo ,pamoja na Biblia kama wanavyo fanya wanawake,ambapo Umoja wa Wanawake katoliki ( WAWATA ) Jimbo la Songea walitoa vipaji katiba Ibada ya PASAKA.

No comments:

Post a Comment