Thursday, March 28, 2013

IBILISI A ANA NJIA ZAKE ZA KULISAMBALATISHA TAIFA LA TANZANIA

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea Norbet Mega Kwenye ibada ya Pasaka
 Askofu Mtega akianzaIbada ya Alhamisi Kuu leo Mjini Songea
 Askofu Mkuu Norbet Mtega akiwa Altareni
 Askofu Mtega akitoa baraka
 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea Dkt Norbet Mtega akipokea vipaji siku ya Alhamisi kuu.

Mishumaa
 
 


ASKOFU Mkuu wa Jimbo kuu la Songea Mhashamu Norbet Mtega amelitahadhahaisha Taifa kuwa Ibilisi wamaingia nchini ili kulisambalatisha taifa ambalo lina amani na ushirikiano wa wakazi ambao wanashirikiana kwa kila jambo kutokana na mshikamano waliokuwa nao.
Askofu Mtega alisema Ibili ana njia nyingi za kulisambalatisha taifa hilo,kwani mambo yamekuwa yanazidi ya kutishia waumini wa madhehebu wa Dini ya Kikristo waogope kwenda kuabudu kwenye nyumba za Ibada kwa ajili ya kumwogopa  ibilisi ailiyoingia nchini.
Alisema Ibilisi hawafurahii,Uhuru,Muungano,Ushirikiano na umoja tuliokuwa nao, bali wanataka kuturudisha katika utumwa, na kila mmoja anaelewa athari za utumwa, hivyo utumwa huo unataka kurudi kama si wao ni watoto wao au wajukuu wao.
Aidha alisema kuwa sumu inayoingia katika taifa kwa kupitia ibilisi, ni adui wa Uhuru wetu,Muungano wetu,Ushirikiano wetu na mshikamano wetu ambapo Wakristu na Waislamu walikuwa akishirikiana katika shida na raha sasa Ibilisi anatumia njia zake kuusambaratisha umoja uliopo.
Alisema tuwaombee viongozi wa Taifa hili,waweze kuliongoza taifa kwa upendo,amani umaoja na mshikamano uliyopo na kujaribi kukemea matendo ya kiibisili yanapojitokeza.

Askofu alisema hayo wakati wa mahubiri wakati wa Ibada ya Alhamisi kuu,katika kanisa kuu la jimbo Kuu la Mtakatifu Mathias Mulumba Kalemba Manjispaa ya Songea leo.
 

No comments:

Post a Comment