Friday, March 29, 2013

TAIFA LIMETAKIWA LISICHANGANYE MASUALA YA KIDINI NA KISIASA

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea Dkt Norbet Mtega akitoa baraka Jana



KATIKA Ibada ya Ijumaa kuu iliyoanyika katika kanisa la Jimbo kuu la Mtakatiu Mathias Mulumba Kalemba la Mjini Songea,ambapo waumini wa Romani Katoliki waliungana na wenzao Duniani Kote,kukumbuka siku ambayo Yesu Kristu alipotiwa mikononi kwa Ibilisi na kusulubiwa na kufa kwa mateso makali  na kufufuka siku ya tatu.

Askofu Mkuu wa Jimbo hilo Dkt.Norbet Mtega alisema katika mahubiri yake,kuwa Taifa la Tanzania lisichanganye masuala ya kidini na kiyasiasa,kwa kufanya hivyo haki haitatendeka kwa jamii ya taifa hilo.

Dkt .Mtega alisema kuwa viongozi wa dini zote wawahubiliea waumini wao maadili mema ya upendo  na amani baina ya dini zenyewe kwa zenyewe na dini nyingine, Serikali iwasaidie kuhamasisha amani na upendo kwa dini zote,kwa kufanya hivyo hakuna dini itakayo kuwa juu ya dini nyingine.kwa kuwa wote tuna mwamini Mungu Mmoja.

Aidha alisema Madaraka yatolewe kwa kufuata Katiba ya nchi,na yasitolewe kwa kufuata kuelewana,udugu,urafiki,ujomba kwa kufanya hivyo wananchi hawatatendewa haki,unyonge utazidi endelea kwa wale wasiyo kuwa na ndugu katika ofisi hizo.

Alisema Pasaka hii ni ya mwaka wa Imani kwa Kanisa,kwa hiyo waumini katika Pasaka hii waliombee taifa hili amani na upendo.Wafanye maombi kwa ajili ya viongozi wanchi na watu wake.

No comments:

Post a Comment