Sunday, April 22, 2012

SIKU MAKA YA JUMAPILI YA LEO YESU KRISTO ALIWATOKEA MITUME WALIMO JIFUNGIA KWA HOFU, AKAWAAMMBIA AMANI IWE KWENU.

Yesu Kristo alipowaambia wafuasi wake amani na iwe nanyi,ile inamaana yeye mwenyewe ana amani na wanadamu ambao amekufa kwa ajili ya dhambi na udhaifu wa kibinadamu walio kuwa nao.Hivyo na waumini wa Roman Catholic wakati wa matoleo Padre husema kwa waumini wake kuwa mtakiane amani.Na waumini hupeana mikono kwa kutakiana amani. Je waumini wote wana amani mioyoni mwao?
  Mchungaji mmoja katika mahubiri yake alisema,unapo mtakia mwenzako amani ,wewe mwenyewe uwe na amani moyoni mwako,vinginevyo unamtakia mwenzako hasira.kwa kuwa amani imetoweka miongoni mwa jamii,ukweli na uwazi haupo,dunia imajaa vita,dhuluma,unyanyasaji.Amani hakuna,watu wanakimbia nchi zao wanaisha uhamishoni,na kuwa wakimbizi,tatizo hakuna amani.

1 comment: