Thursday, January 31, 2013

UBABE WA WAFUGAJI WA KIMASAI UNAENDELA PALE WALIPO MSHAMBULIA MKULIMA WA KIJIJI CHA KIMAMBA KILOSA KWA FIMBO NA KUMJERUHI MIKONO YAKE ALIPOULIZA KWA NINI NG'OMBE WANAKULA MAHINDI YAKE

Mkulima mmoja wa kijiji cha kimamba kilosa Mkoani Morogoro Mzee Ally Mkakari jana amepata kipigo kutoka kwa wafugaji wa Kimasai ambao waliwaingiza ng'ombe wao kulisha shamba lake.
Mzee Ally alisha peleka malalamiko yake kuhusu shamba lake kushambuliwa na wanyama.lakini hakupata jibu lolote kutoka Kituo kidogo cha Polisi Kimamba.Kiukweli wamasi ni wababe wanaingiza ng'mbe kwenye mashamba ya wakulima kwa makusudi,mkulima akiuliza anapata mkong'oto hata kutotolewa uhai wake na wafugaji hao.Na uongozi wa Wilaya na Mkoa unangalia tu,hivyo kwanini wakulima wanakuwa wanyonge kwa wafugaji hao? Je wanatoa kitugani kwa uongozi wa wilaya na Mkoa? hali hiyo itaendelea hadi lini?
Kwanini wasitengewe maeneo yao wafugaji hao ,ili kunusuru uhai wa wakulima na mali zao.

No comments:

Post a Comment