Saturday, June 9, 2012

SAFARI HII YA KIKAZI LINDI NA MTWARA NIMEJIFUNZA MENGI.

 Wenyeji wa Mji wa Lindi wanajishughulisha na ukusanyaji wa chumvi na kuiwekea mqdini joto,wajipatia kipato kutokana na kazi hiyo.
 Jioni nilikuwa natokea zangu bandarini Lindi mjini kuona jinsi majengo ya bandari hiyo yalivyo telekezwa
Hilo nalo ni eneo jingine ambalo chumvi inakusanywa na wakazi hao wa Mji wa Lindi,chumvi ambayo soko lake liko Dar es Salaam.
 Huyo na Mwanataaluma wa habari Kanda ya Kusini katika shughuli za kikazi Mtwara na Lindi Bw.Juma Nyumayo akiwa anaondoka kutoka Kilwa Masoko na Kuelekea Kilwa Kivijne kuendelea na shughuli hivi karibuni.
Hizo na ofisi za Bandari ya Lindi ambayo imetelekezwa,haifanyi kazi kama mwanzo ambapo meli zilikuwa zikitia nanga katika bandari hiyo.
Hilo na baadhi ya majengo yaliyojengwa enzi ya utawala wa kisultani mwambao wa Pwani ya Afrika mashariki,Hiyo miti siyo mapambo bali ni miti iliyoota ndani ya jengo na kubomoa kuta zake,Utalii usisubili wazungu kuja kuoana maajabu ya kale,na jinsi babu zetu walivyo weza kujenga majumba bila ya kutumia sementi au tofali.
 Nilikuwa nashangaa kuona mchanga ulivyo jaa kwenye eneo ambapo meli zilikuwa zikitia nanga enzi zake za MV Lindi ikitamba baharini siku mbili kutoka Dar es Salaam hadi Lindi,Tiketi unaisotea wiki mbili kwa bei ya halali Mlango wa nyuma siku moja au mbili unasafiri,Hizo hapo ni meli ambazo zinakarabatiwa ziludishwe Zanzibar.
 Pwani ya Lindi jioni watu wanapunga upepo
Wengine wanaogelea,wanacheza basi mradi wanajiburudisha kwenye bahari ya maji ua chumvi,hiyo ndiyo safari yetu na Bw.Nyumayo mikoa ya Mtwara na Lindi tutaendelea kipindi kijacho.

No comments:

Post a Comment