Monday, January 30, 2012

Wazazi kuchangia chakula shule ya sekondari Kalembo WAZAZI wa wanafunzi wanaosoma katika shule ya sekondari Kalembo Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wanachangia sh. 30,000 kwa muhula kwa ajili ya kupatiwa chakula cha mchana na uji wakati wa asubuhi,ingawa kiasi hicho hakitoshi. Mkuu wa shule ya sekondari Kalembo Bwana Bosco Haule alizungumzia umuhimu wa kutoa chakula kwa wanafunzi wanaosoma shule za msingi na sekondari mkoani hapo na nchi nzima kwa ujumla alipoitembelea ofisi za TUJIFUNZE leo. Bw.Haule alisema kuwa utaratibu wa kutoa chakula katika shule yake haukuanza hivi karibuni,bali ulianza toka mwaka 2005,kwa kutumia Bodi ya shule kuwahamasisha wazazi wenye watoto ambao wanasoma katika shule hiyo kwa kuchangia sh.30,000 kwa muhula. Alisema mchango wa sh.30,000 kwa muhula kwa kipindi hiki akitoshi,lakini kwa kubana matumizi wamefanikiwa kutoa uji na chakula cha mchana ,ambacho ni ugali kwa maharage,ingawa bei ya maharge hayo iko juu ikilinganishwa na bei ya mahindi katika mkoa wa Ruvuma. Kuhusu walimu Bw.Haule alisema walimu nao ili waweze kufanya kazi kwa usahii,na wao wanapata chai na chakula cha mchana kwa kuchangia sh.10,000 kila mmoja. Aidha Mkuu wa Shule huyo alisema kuwa kwa wanafunzi ambao wazazi wao hawakuchangia fedha au nafaka kwa ajili ya chakula

Mkuu wa shule ya Kalembo liyoko Matogoro nje kidogo na Manispaa ya Songea Bwana Bosco Haule akielezea jinsi alivyo fanikiwa kuwapa chakula cha mchana wanafunzi wa shule yake.Ansema ili chakula kipatikane shuleni ni vyema kufanya mikutano na wazazi wakubaliane kuchanga fedha na kiasi cha kuchangisha kwa kila mzazi.



WAZAZI wa wanafunzi wanaosoma katika shule ya sekondari Kalembo Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wanachangia sh. 30,000 kwa muhula kwa ajili ya kupatiwa chakula cha mchana na uji wakati wa asubuhi,ingawa kiasi hicho hakitoshi.

Mkuu wa shule ya sekondari Kalembo Bwana Bosco Haule alizungumzia umuhimu wa kutoa chakula kwa wanafunzi wanaosoma shule za msingi na sekondari  mkoani hapo na nchi nzima kwa ujumla alipoitembelea ofisi za TUJIFUNZE leo.
Bw.Haule alisema kuwa utaratibu wa kutoa chakula katika shule yake haukuanza hivi karibuni,bali ulianza toka mwaka 2005,kwa kutumia Bodi ya shule kuwahamasisha  wazazi wenye watoto ambao wanasoma katika shule hiyo kwa kuchangia sh.30,000 kwa muhula.
Alisema mchango wa sh.30,000 kwa muhula kwa kipindi hiki akitoshi,lakini kwa kubana matumizi wamefanikiwa kutoa uji na chakula cha mchana ,ambacho ni ugali kwa maharage,ingawa bei ya maharge hayo iko juu ikilinganishwa na bei ya mahindi katika mkoa wa Ruvuma.
Kuhusu walimu Bw.Haule alisema walimu nao ili waweze kufanya kazi kwa usahii,na wao wanapata chai na chakula cha mchana kwa kuchangia sh.10,000 kila mmoja.
Aidha Mkuu wa Shule huyo alisema kuwa kwa wanafunzi ambao wazazi wao hawakuchangia fedha au nafaka kwa ajili ya chakula cha watoto wao,hawapati chakula,ili wazazi wenye watoto hao waone umuhimu wa kupata chakula kwa wanafunzi.Nakwamba kila mwanafunzi anatumia sh.350/=  kwa siku.

ONA CLIP NILIYOIPATA KWA KARIBU KWENYE AJALI HIYO WAKATI BUS LETU LINAPITA ENEO LA TUKIO

Clip au video hiyo inaonyesha kipande cha tukio kilivyo tokea,bus hilo lilitangulia hapo jana  nasi tuli kuwa nyuma na Bus la Summry ya kwenda Songea wakati nikitokea Dar es Salaam kutoka Kilimanjaro nikokuwa kikazi kwa wiki moja.

Sunday, January 29, 2012

Mvua na zinazonyesha za sababisha ajali ya New Force Bus liendalo Mbeya kutoka Mbeya jana

i
 Eneo hilo la Nyololo kilometa chache kufika Makamabo Mkoani Iringa ni eneo baya hasa wakati wa mvua kuna utelezi sana.jana siku ya Jumamosi Basi  ' bus' New Force one lilokuwa likitokea Dar es Salaam lilipinduka,na kusababisha ajali.kwa kuwa Bus letu La Kampuni ya Sumry lilisimama mbali kidogo na Tukio ,ndiyo maana picha ya jirani haikupatikana.kama unavyoona juu kwenye malori ndipo kwenye ajali.
Lakini utaona clip hiyo niliyoipata  bus letu lilipo simama. kwa hiyo madereva wanapaswa kuwa waangalifi wakati wa 'overtaking lorries' wakati wa mvua na kwenye miteremko.

Friday, January 27, 2012

USEMI WA BONGO NIMEUSHUHUDIA LEO HAPA JIJINI DAR ES SALAAM

 Mpiga picha wa Blog hii leo alipata nafasi ya kuona jinsi wabongo wanavyo jishughulisha na maisha,hapo ni eneo la Feri Jijini Dar es salaam maarufu kwa uzaji wa samaki wabichi pia wanaokaangwa.wakazi  wengi wanatoka kila pembe ya Jiji hilo kufika hapo kwenda kununua samaki wa kwenda kuwauza baada ya kuwakaanga,wasomesha watoto wao,wanajenga,aidha mahitaji yo yote muhimu wanapata kutokana na shughuli hizo,' Hiyo ndiyo bongo'
 Pilika pilika foleni ya magari ni kitu cha kawaida hasa muda wa asubuhi watu wanakwenda kazini na muda wa kurudi kazini.Hapo ni maeneo ya Manzese  Dar es salaam.
 Wanafunzi wasukuma mikokoteni ya kuuzia maji nao wako katika harakati ili mradi wawahi kwenye maeneo husika.Mpiga picha aliwakuta hao maeneo ya Mabibo Jijini Dar es salaam Leo.
Wenye baiskeli na watembea kwa mguu katika Jiji hilo ni wengi kushinda wanaokuwa kwenye usafiri,Lakini yote ni mema Jiji au mji hauwezi kuwa na sifa kama watu wa ina na nafasi tofauti watakosekana wote kwa pamoja ndiyo wanaofanya Jiji liitwe hivyo.


JIJI la Dar es Salaam wameliita bongo kutokana na watu wa Jiji hilo hutumia akili sana ili waweze kuishi katika Jiji hilo liitwalo Dar es Salaam,maana si dhani watu hao wana lala saa ngapi maana magari usiku kucha yanapita kuelekea yaendako  na yale yatokako.Mkazi mmoja hakupenda jina lake lijulikane maeeneo ya Feri ambako asilimia kubwa ya wakazi wa Jiji  Hilo ndipo wanapo patia maisha yao,alisema .
‘ Saa  kumi ya usiku kuna baadhi ya wafanyakazi wanaamka kujiandaa kwenda kwenye vituo vya daladala,na wengine wanajiandaa kuja hapa Feri kuwasubiri wavuvi kutoka kuvua samaki ili wanunue waende kuwakaanga na kuwauza,na asilimia kubwa ni akina mama.’
Lazima kutumia akili,kwenye uzalishaji mali ujasiliamali mdogomdogo,biashara za kuuza maji,matunda,mboga,Juisi,vyakula,plastiki za maji vyuma chakavu mama na baba ntilie.
Pia wapiga debe,waombaji,matapeli wanaotumia bongo zao kujifanya maofisa wa serikali au shirika Fulani,wanaojifanya wanauza simu ama saa za bei mbaya ,ambao wamewaliza wasafiri wengi Stendi kuu ya  mabasi yendeyo mikoani .Ubungo kwa kuwauzia vipande vya sabuni ama kibao wamevifunga  kwa ustadi kwenye bahasha ya kaki na kumkabidhi msafiri kwenye basi anapo fungua anakuta sabuni au kibao basi,Jamaa anatokomea mkwenye mabasi.hiyo ndiyo bongo.
Kwa utaratibu huo wasafiri wanatakiwa wawe macho,simu na saa mbona zimejaa madukani siku hizi! Kwa nini unataka ‘short cut’waogopeni sana watu hao sanacho kuonyesha sicho atakacho kukukabidhi baada ya kumpa fedha hata angevaa na kuwa nadhifu kiasi gani Wabongo hao.Samahani sio samaki mmoja akioza ndiyo wote hapana ila baadhi ya Wa – Bongo ni wajanja.  

Wednesday, January 25, 2012

MADHARI YA MANISPAA YA MOSHI MJI MSAFI KATI YA MANISPAA NILIZO TEMBELEA

Milipokuwa katika Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro,kwenye Round about yao ambapo mbele kuna jengo La Chama kikuu cha Ushirika Moshi ( KNCU ).
Aidha nikaenda tena kwenye Stand kuu ya mabasi yaendayo mikoani Moshi Mjini.
Huo ni mji wa Manispaa ya Moshi unavyo onekana.

Monday, January 23, 2012

NI MUDA MREFU SIPO KWENYE MTANDAO,WASOMAJI WA BLOG HII NIKO KIKAZI MKOANI KILIMANJARO

 Mt Kilimanjaro ni mlima mrefu katika Afrika nipo huku
 Kibo mountain at Kilimanjaro Tanzania another Mawenzi not seen.
Tujielimishe Kanda ya Kaskazini Moshi Kilimanjaro  Mhariri wa Kanda hii ni Bibi Josephine Sanga Niko naye tunafanya kazi muhimu ya Kanda hii.

Friday, January 13, 2012

MADHARI YA MIJI YA DODOMA NA MOROGORO YANAVYO VUTIA WAGENI KATIKA UPANDAJI WA MAUA

 Kabla ya kuingia stand kuu ya mabasi katika Manispaa ya Dodoma utakutana na 'roundabout' hiyo ndipo utaingia katika Stand ya mabasi.
 Lakini ukiwa karibu na 'roundabout' hiyo mbele yako utaliona jengo la ukumbi wa Bunge linalo onekana mbele ya miti

Na hapo chini ni 'round about' mjini Morogoro baada ya kuipita 'roundabout' ya Stand kuu ya mabasi Msamvu.Ama kweli maua yanapendezesha mji kama yatatunzwa vyema.

Do you agreed with Shannon and weaver’s model ,and Wilbur Schramm and the Berlo Model. Argued that communication is not without barriers


.
Those scholars said that the barriers are related to:-
·        Lack of knowledge
·        Distraction
·        Lack of concentration
·        Education background
·        Physical impairments
·        Emotions and attitudes
·        Age
·        Socio-economics status and
            Appropriateness

Thursday, January 12, 2012

BAADA YA KAZI NI KUJIBURUDISHA NA VINYWAJI BARIDI

 Baada ya shughuli zangu tulitulia kwenye duka moja tukapata soda baridi,tukiwa na Kaka yangu Mzee Ally  mwenye kofia na Dada yangu Mrs Mnose,kimamba kilosa hivi karibuni.
 Hao ni dada Mrs mnose,kaka yangu Mzee Ally na aneno Mziwanza wote wa Kimamba wakipata soda,
Wakiwa wakibadilishana nawazo baada ya kupata soda.

Nilipokuwa Kimamba Kilosa Mkoa wa Morogoro baada ya Likizo yangu Nikutana walimu

 Ni picha ya pamoja ya walimu,mwenye kofia mwalimu Mnose na wa pili mwenye suluwali nyeusi ni mwalimu mkuu Bwana Kajika Gallan wote wa shule ya msingi Usagara Kimamba - Kilosa
 Bwana Mnose
 Bwana Gallan
 Bwana Mnose na shemeji yake Bi.Christina Hilaliyo
Mwalimu mkuu Bwana Kajika Gallan akiwa ofisini kwake

LIKIZO NILIVYOITUMIA NIKIWA NYUMBANI DODOMA ILOANDAMANA NA UKARABATI WA NYUMBA YANGU ILIYOTEKETEA NA MOTO TAREHE 28/12/2011 MANISPAA YA DODOMA

a
 Sintosahau siku ambayo Mke wangu na mjukuu wangu Sara na mama mkwe Coleta ambayo wangepoteza maisha yao kwa kifo kibaya cha moto,ukliyotokea tarehe 28/12/2011 saa 1.30 usiku,moto uliyoanzia sitting room na dining room wakati Mrs Sikapundwa akiwa ndani na watoto wakiwa chumba kingine,ambapo mama huyo aliskia mlio kama bom,kumbe zilikuwa TV vikipasuka ndipo alipo gundua kuwa hatari.Mama ni yule mwenye nguo nyeupe na Sarah ni yule aliyeshika kiuno.
 Nilikuwa nashangaa jinsi moto ulivyo tekekteza mlango na dirisha.ama kweli kama siku za kufa mtu bado ,chuki na hila za binadamu haziwezi kufua dafu.Lakini watu husema kwa nini kumwingilia Mungu kazi yake?,kazi ya kuua ni ya Mungu peke yake,wengine wanamwingila.
Ukianagalia miujiza ya Mungu ,huwezi amini,kwenye ngzi ndogo kuna dirisha la blue,basi kwenye dirisha lile ndipo Mke wangu Mrs E.Sikapundwa alipovutwa na watu waliyofika kwenye tukio hilo siku hiyo ambayo shetani alitawala katika nyumba ile,lakini Mungu alikataa.
Nawashukuru majirani,Kikosi cha kuzima moto cha Manispaa ya Dodoma,Walimu wa shule za msingi za manispaa hiyo hususani shule ya msingi Makole ambapo mama huyo anafundisha hapo,Jumuiya tunayosali ya Makole na watu wote waliyoziokoa roho za wanafamilia yangu.sina cha kuwalipa bali na sema asante,

BREAKIN G NEWS AFGHANISTAN

Car bomb kills five people including distrhict governors,in south Afghanistan.

Wednesday, January 11, 2012

MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA ZINASBABISHA USAFIRI WA MABASI YAENDEYO KILOSA NA KURUDI MOROGORO KUWA MGUMU KUPITIA MELELA,MKATA,KIMAMBA HADI KWA KUWA NA BARABARA YA VUMBI KWA MIAKA KADHAA SASA

a
 Basi hilo limeharibika katika maeno ya Mkara Ranch ,kutokana na mvua zilizonyesha mfululizo na kusababisha barabara kuwa na matope,na kwamba magari mengi yanakata spring.
 Hilo ni basi ambalo nalo limekata spring lilivyoingia kwenye mashimo maeneo ya Faruma si mabli sana kutoka Kimamba.wamiliki wa mabasi hayo wanashindwa kuelewa kwa nini serikali inashindwa kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami?
Hiyo ndiyo barabara ya kutoka kilosa kupitia Kimamba,Mkata ,Melela hadi Morogoro,eneo hilo ndilo safi kidogo,isitoshe hata ukarabati haupo kwenye barabara hiyo,haijulikani ni kwa sababu haijatengewa fedha za Tan road za matengenezo,ama Halmashuri au Mkaoa wenye jibuni Waziri mwenye dhana lakini pia na Mbunge wao wa Kilosa,anaona na anapita kwenye barabara hiyo nadhani hata ifimbia macho barabara hiyo ilwe kwenye kiwango cha lami.

kilio cha wakulima wa Wilaya ya Kilosa,kinagonga mwamba kila mara kwa uongozi wa Wilaya hiyo wanapopeleka kesi za kuliwa mazao yao na ng'ombe wa wafugaji wa kimasai

 Makundi kwa makundi ya ng'ombe wa wafugaji wa kabila la wamasia yamekuwa kero na hasara kubwa kwa wakulima wa wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro.
Wakulima wa Tarafa ya Kimamba,Madoto,Rudewa Msowero, wanapata shida sana na wafugaji hao ambao wanalisha ngombe wao kwenye mashamba ya watu kwa makusudi.'mashamba tuna kodishwa kwakuwa maneo tunayolima na mashamba ya mkonge ya mwei wa kukezaji,wakati  mazoa yakikomaa wamasai wanaingiza ng'ombe zao kulisha,ukipeleka kesi hiyo kwenye uongozi wa wilaya wanakuambia nenda tunashughulikia,utapigwa kalenda,kwa kuwa wamasai hao wana fedha za kutoa kwa wakubwa na wakulima hatuna kitu.' walisema wakulima hao ambao hawakupende majina yao yajulikane.na kwamba walisema viongozi wa ngazi zote wananufaika na kuliwa kwa mazao ya wakulima ktika wilaya hiyo.
Jeuri ya fedha inawapa kichwa maji wamasai wafugaji,wakulima walala hoi wanambulia patupu,Ukweli Serikali ijaribu kuangalia hakiza wa wakulima hao,bila ubaguzi wa nani ana fedha na mwengine hana basi akose haki yake,ndiyo kila mika kuna kuwa na mapigano kati ya wakulima na wafugaji hao katika wilaya hiyo.

SERIKALI IJARIBU KUIOKOA RELI YA KATI ,HALIYA RELI HIYO INASIKITISHA,TRAIN KUPITA KWENYE RELI ILIYO GUBIKWA NA NYASI NI HATARI ,HAKUNA USALAMA

Hiyo ni reli ya kati katika station ya Kimamba Kilosa Mkoa wa Morogoro,hali kama hiyo hapo ni station je katikati ya mikoa ya Dodoma,Tabora,Kigoma,shinyanga na Mwanza hali iko vipi.,Kama mwekezaji yupo basi ifanye jitihada ya kuwarudisha wafanya kazi wa magenge mabo mwanzo walikuwa wanaita pigilia,amabo walikuwa wakifanya usafi katika reli hiyo na wakaguzi wa reli,ili kuwe na usalama wa train. lakini sasa hawapo hao,kwa utaratibu huo ajali zitakosekana?
Reli ya kati ni muhimu sana kwa kusafirisha mizigo kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma,Mwanza na kurudisha mizigo mingine,aidha ilisaidia sana wasafiri amabo hawana kipato cha kutosha ,hasa nauli za mabasi,Hebu serikali hasa wizara ya miundo mbinu ijariku kulikwamua shirika hilo kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

MUHULA WA MASOMO KWA SHULE ZA MSINGI UMENZA JUMATATU WIKI HII KATIKA SHULE YA MSINGI USAGARA KIMAMBA KILOSA WANAFUNZI WANAONEKANA WENYE FURAHA

 Ni saa moja na nusu asubuhi ya Jumatatu wiki hii wanafunzi wa shule ya msingi Usagara Kimamba Kilosa Mkoa wa Morogoro wakiwa kwenye sare zao za shule kutoka awali wenye sare za kijani hadi darasa la saba wakiimba wimbo wa Taifa na wimbo wa shule ,wakiwa na walimu wao wakiwa na ari ya kuanza ngwe ya kwanza ya kazi yao ya kuelimisha Taifa hili.
 Wanafunzi wa Awali wakiwa na kaka na dada zao kwenye mistari ,tayari kwa kuingia madarasani.
 Hao ni wanafunzi wa darasa la saba ambao wanaingia darasa hilo kwa mara ya kwanza kutoka darasa la sita.
 Baadhi ya walimu wa shule hiyo waliyo kutwa na blog hii asubuhi hiyo wakiwa wakisubiri wanafunzi kuingia madarasani ili wakafanye kazi yao ya kufundisha.Ambapo hapo awali kazi hii nyeti ilikuwa ni kazi ya wito,bali sasa imekuwa ni kazi kama kazi nyingine,wanaingia hata wale wasiyo na wito kwa kuwa walikosa kazi.walimu kama hao wanakosa maadili ya ualimu.
Baadhi ya wanafunzi wa darasa la saba waliyokuwa wakifanya usafi kwenye ofisi ya mwalimu mkuu wakijisifia kuwa waote watafaulu mtihani,shule hiyo ina wanafunzi 65 wa Awali na 540 wa shule ya msingi na kufanya idadi ya wanafunzi 605.

Sunday, January 1, 2012

NAWATAKIENI HERI KWA MWAKA MPYA 2012 UWE WENYE AMANI ,UTULIVU,NA FARAJA DUNIANI,MSHIKAMANO WA WATU WALIYOKATA TAMAA YA MAISHA .

NI muda mrefu kiasi sijaonekana katika mtandao wa Blog TUJIFUNZE KUSINI kwakuwa  ni ko likizo  nyumbani Dodoma.ambako niliunguliwa na nyumba hivyo umeme nategemea kesho au kesho kutwa tutakuwa sote hewani
 Nawatakieni Jumapili njema ya mwaka mpya wa 2012  juma la kwanza la mwaka  mpya.