Sunday, December 2, 2012

Meya wa Manispaa ya Songea  Mstaiki Charles Mhagama amewataka wananchi na wazazi wa Manispaa yake kuwapeleka watoto wao wadogo kwenye shule za Awali ,ili wajengeke na msingi mzuri wa kujifunza.
Meya Mhagama alisema hayo katika mahafari ya shule ya Awali Charity iliyoko katika Uwanja wa sabasaba Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma jana,na kwamba katika harambee iliyofanyika katika mahafali hayo,Mstahiki Meya Mhagama aliahidi kutoa malori mawili ya mchanga yenye thamani ya shilingi laki tatu ( 300,000/= ),ambapo Yusufu Kufakunoga,kwa niaba ya Mhariri kanda ya kusini aliahidi kuchangia mifuko mitatu ( 3 ) ya sementi,Mtangazaji wa Star TV Songea Bwana Adam Nindi aliahidi kuchangia Shilingi 20,000/=.
Watoto 13 wamehitimu mafunzo ya Awali,ambapo mwakani watoto hao wataingia darasa la kwanza.Katika picha,wakwanza mwenye suti ya bluu ni mwalimu mkuu,pia ni mkurugenzi wa shule hiyo anayemfuatia mwenye kaunda suti mikono mifupi na Mstahiki Meya Charles Mhagama akimkabidhi cheti mmoja wa wahitimu.

No comments:

Post a Comment