Friday, December 21, 2012

WASICHANA WA FANYA MAAJABU KATIKA MATOKEO YA DARASA LA SABA MWAKA 2012 KWA ASILIMIA 8.8 KWA KUWAPIKU WAVULANA




WAZIRI wa  Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe.Dkt Shukuru Kawambwa  ametangaza matokeo ya darasa la saba mwaka 2012 ofisni kwake kwa waandishi wa habari na kusema wasichana wamefanya vizuri kuliko wavulana kwa asilimia 8.8,baada ya kuongoza kwa asilimia 50.20 kwa kuwapita wavulana kwa asilimia 49.80.
   Waziri huyo alisema kuwa wanafunzi 560,706 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule za serikali,na kati yao wanafunzi 281,460 ni wasichana na 279,246 wavulana ambapo imefanya idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kuongezeka kwa asilimia 8.8, ikilinganishwa na wanafunzi 515,187 ya waliyochaguliwa mwaka uliyopita.
  Mhe. Kawambwa alisema mtihani wa mwaka huu umefanyika kwa mara ya kwanza kwa kutumia Teknolojia mpya ya ‘ optical mark reader’ ambao usahihishaji wake hutumia compyuta,njia ambayo imeipunguzia serikali gharama ikilinganishwa na mwaka jana.
   Alisema kuwa mwaka jana walimu 4,000 walitumika kusahihisha zaidi ya mwezi mmoja,ambapo mwaka huu 285 ndiyo walitumika kwa siku 15 kukamilisha kazi yote.
     Kuhusu matokeo hayo amesema kuwa alama ya juu kabisa ni 234 kati ya 250 kwa wavulana na wasichana, ambapo wanafunzi 3,087 wamepata alama daraja la ‘A’ na wanafunzi 40,683 alama daraja la ‘B’,wanafunzi 222,103 alama daraja la ‘C’ na wanafunzi 526,397 alama daraja ‘D’ ambapo waliobakia 73,264 alama daraja ‘E’
   Aidha alisema vitendo vya udaganyifu vimepungua kutoka wanafunzi 9,736 waliofutiwa matokeo yao mwaka jana ikilinganishwa na wanafunzi 293 waliofutiwa matokeo yao mwaka huu.

No comments:

Post a Comment