Monday, December 31, 2012

WATANZANIA TUPO WATU 44,929,002,AMBAPO TANZANIA BARA 43,625,434 NA ZANZIBAR WATU 1,303,568 ATANGAZA RAIS KIKWETE

 Mhe.Dkt Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua Sensa ya watu na makazi Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam leo atangaza  Kuwa Tanzania ina watu 44,929,002.Tanzania Bara watu 43,625,434 na Zanzibar watu 1,303,568.
 Waziri wa Fedha Mhe, Wili
Mkamu wa Rais Zanzibar Mhe.Balozi Seif Ali akielezea mafanikio ya zoezi la Sensa mwaka 2012
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pia mwenyekiti wa Sensa Taifa akielezea mafaniko ya sensa hiyo katika viwanja vya Mnazi mmoja Jijini Dar es Salaam leo.
 Mariam Kan Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa akielezea jinsi Tanzania ilivyofanikisha zoezi hilo kwa malengo ya kupanga bajeti  kwa maendeleo ya nchi.
Msomaji wa Utenzi Bi Amina Haji kutoka Zanzibar katika viwanja vya Mnazi mmoja Jijini Dar es Salaam Leo.


RAIS  KIKWETE  ATANGAZA MATOKEO YA AWALI YA SENSA YA WATU NA MAKAZI  KUWA TANZANIA INA WATU 44,929,002 KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA LEO, TAREHE 31 DESEMBA 2012 DAR ES SALAAM

RAIS Kikwete alisema kuwa uzinduzi huu wa awali siyo kuwa kuna matokeo mengine la bali yamekamilika isipokuwa mwezi Februari 2013 kutakuwepo na matokeo ya idadi ya watu kijinsia.kujua wanaume ni wanagapi na wanawake ni wangapi.
Alisema kuwa katika matokeo hayo,Tanzania Bara kuna indadi ya watu  43,625,434 na Zanzibar kuna watu 1,303,568.
Aidha alisema pamoja na changamoto kadhaa zilizojitokeza lakini zoezi hilo limefanikiwa kwa asilia 90.
Baadhi ya changamoto hizo ni pamoja na maandamano wakati wa zoezi liliendelea,watu kujifungia ndani kwa kukataa kuhesabiwa.
Alisema matokeo ya idadi ya watu imeonyesha jinsi watu wanavyoongezeka, na kwamba mwaka 2016 idadi ya Watanzania itakuwa 51,600,000,hivyo ni mzigo mkubwa kwa Taifa na Serikali pia na jamii kwa ujumla.Hivyo serikali itapanga mipango yake ya maendeleo ili kukabiliana na idadi kubwa ya watu,lakini pia watanzania wafuate uzazi wa mpango kwa lengo la kuzaa watoto ambao wataweza kuwahudumia.

No comments:

Post a Comment