Sunday, December 23, 2012

NYAISONGA AWAPA MAADILI YA KIDINI WATOTO WA KIPEMARA DODOMA

 Baba Askofu Grevasi Nyaisonga wa Jimbo la Dodoma akitoa mahubiri kwenye maazimisho ya misa Takatifu ya Kipeimara katika Parokia Ya Mt Kalori Lwanga ya Makole Katika Manispaa ya Dodoma.
 Baadhi ya watoto waliyopata Kipeimara leo katika Parokia ya Makole leo.
 Waumini waliohudhuria ibada hiyo ya Kipeimara leo
Ni kwa ya Mtakatifu Kalori Lwanga ya Makole ikiinjisha kwa nyimbo katika ibada iliyofanyika leo Parokiani hapo.
 Askofu akitoa Kipeimara kwa kumweka Ishara ya Msalaba kwa mafuta na kofi shavuni .
 Wakiwa katika mageuzi ya mkate na divai
 Akionyesha kikombe cha divai kama ishara ya Damu ya Yesu,iliyo mwangika kwa ajili ya wengi kwa maondoleo ya dhambi
a
 Askofu Nyaisonga akimpa mkono mmoja wa waumini waliyo hudhuria misa hiyo leo.
Askofu Nyaisonga akitoa Baraka kwa waumini kanisani humo baasa ya Ibada hiyo hivi leo.


WATAKIWA KUISHI KWA IMANI KWA KUYASHINDA MAGUMU KATIKA MAISHA WATOTO WA KIPEIMARA DODOMA

ASKOFU wa Jimbo la Dodoma Mhashamu Grevasi Nyaisonga ,amewataka watoto waliopata Kimeimara wawe mashaidi wa Yesu Kristo kwa vitendo kwa ndani na nje,hasa katika kufuata imani ya kweli ya upendo  mbele za Mungu na watu  wote.
Baba Askofu Nyaisonga alisema kuwa kipemara kimewapa nguvu ya kuyashinda magumu katika maisha yao kwa mapenzi ya Mungu na kuwafanya askari imara wa Mungu kwa kuwa mashuhuda wa Yesu Kristo.
Askofu Nyaisonga ametoa Kipeimara kwa watoto 300 katika Parokia ya Mtakatifu Karoli Lwanga ya Makole katika Manispaa ya Dodoma Mkoa wa Dodoma Leo.
Aidha amesema kuwa katika kuchangia kwaya ya Mt.Kalori Lwanga ya Makole,waumini wanunue kanda zao zenye nyimbi za Unjilishaji za VIDEO,Pia wanunue na Kalenda ambazo zinaweza kuingizia Parokia mapato yake.
Wakati huohuo Mwenyekiti wa Parokia hiyo Bwana Evarist Mnaranara  amemshukuru Baba Askofu kwa kuwapa Kipeimara watoto hao,amewashukuru,Makatekista, na wazazi kwa kuwaandaa watoto hao katika mafundisho ya dini hadi kufikia kupata kipemara hicho.
Pia alisema pamoja na msimu wa mvua ,watu wafanye kazi kwa juhudi kubwa,na wakulima waende shamba maana msimu wa kilimo umeshaanza,kwa kufanya hivyo kutapatikana chakula cha kustosha kwa ajili ya familia zao.

No comments:

Post a Comment