Monday, December 17, 2012

WAKUU WA VITUO VYA KANDA SABA ZA MAGAZETI YA KISOMO WAMETAKIWA KUSIMAMA NA KUJENGA USHIRIKIANO KATIKA UTENDAJI KAZI ZAO

 Mkurugenzi wa Elimu ya Watu Wazima na Nje ya Mfumo Rasmi Bwana Salumu Mnjagila akiwasomea vipengere vya fomu za PRAS   Wahariri wa Magazeti vijijini wa Kanda saba katika ofisi yake  Mkao Makuu ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Jijini Dar es Salaam jana.
 Baadhi ya washiriki katika kikao hicho cha kazi wakimsikiliza Mkurugenzi kwa makini
 Naibu Mkurugenzi Kisomo Mwanza Bibi Mary Joseph Salu
 Picha ya Pamoja ya viongozi wa Idara ya Elimu ya Watu Wazima na Nje ya Mfumo Rasmi na  Baadhi ya wahariri wa magazeti vjijini
 Mkurugenzi Msaidizi Utawala Bw.Gange akitoa mada ya OPRAS kwa Wahariri wa Vituo vya uchapaji




WAKUU  wa vituo wa Kanda  saba  za magazeti ya kisomo  nchini,wametakiwa kusimama kwa ushirikiano na mshikamano wao katika ufanisi wa kazi zao za kuelimisha wananchi kupitia magazeti yao ya kisomo yanayo chapwa katika Kanda zao.
     Mkurugenzi wa Elimu ya Watu Wazima na Nje ya Mfumo Rasmi EWW/ENMRA Bwana salumu Mnjagila alisema hayo wakati wa kikao cha kazi kilicho fanyika ofisni kwake leo Makao makuu ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi JIjini Dar es Salaam.
     Bw.Mnjagila alisema kila mmoja atambue nafasi yake kituoni ili kuleta ufanisi wa kazi bila ya kusababisha migongano baina ya viongozi na watumishi katika vituo hivyo.
Aidha alisema vituo hivyo vitafanya kazi za maendeleo ya kuboresha  elimu nchini iwapo watafanya kazi kwa kuelewana  na kuwa wawazi katika maamuzi ya utekelezaji wa majukumu waliyo jipangia.
     Kikao hicho kilijumuishi Msaidizi Utawala Bwana Gange na Mkurugenzi Msaidizi Ufuatiliaji wa Taaluma Bibi Revilla na Wahariri  wa Vituo vya Uchapaji Magazeti Vijijini vya Mwanza,Tabora,Mbeya na Songea, ambao pia ni wakuu wa vituo hivyo.


No comments:

Post a Comment