Monday, July 30, 2012

MWALIMU APEWA MKONG’OTO NA WANAFUNZI WAKE KWA KUFUNDISHA SIKU YA MGOMO WA WALIMU SONGEA



BADHI ya wanafunzi wa shule ya msingi Kambarage Halmashauri ya Manispaa ya Songea wamempatia mkong’oto mwalimu   aliyejulikana kwa jina la Kahimba kwa madai ya kuwa na kuherehere cha kufundisha wakati walimu wengine wapo kwenye mgomo ulifanyika nchi nzima,wakidai kuwa mwalimu huyo amewasaliti walimu wenzake na viongozi wa Chama cha Walimu Tanzania.
   Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kambarage Bibi Adolophine Ndunguru katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea alithibitisha tulio hilo kuwa lilitokea majira ya asubuhi.
    Aidha Katibu wa Chama Cha Walimu Tanzania wa Mkoa wa Ruvuma Bwana Luya Ngonyani,alisema kuwa Mgomo wa Walimu ni halali umezingatia sheria ya ajira na mahusiano kazini ya mwaka 2004.
     Alisema kuwa hatua ya kwanza ya Chama Cha Walimu  (CWT ) imetekeleza kutangaza mgogoro wa siku 30 kwa kujaza fomu namba 1 kwa lengo la kudai  maslahi yao.
    Wakati Uongozi wa Manispaa ya Halmashauri ya Songea wakitaka kuitisha mkutano wa Waratibu Elimu Kata na Walimu wakuu wa shule wa Manispaa hiyo leo katika shule ya msingi Mfaranyaki uligonga mwamba baadaya wa Waratibu na walimu wakuu hao kuacha kwenda kwenye mkutano huo.
  Serikali isifanyie mzaha kuhusu tukio hilo,sio suala la kusema shauri lipo mahakamani ,walimu warudi shuleni kufundisha,Sekta ya Elimu ni Sekta nyeti si ya kuichezea chazea kama wengine wanavyo dhani,Mwalimu anaweza akapindisha Mtaala wa Elimu akafanya kinyume na Sera ya nchi kwa muda mfupi sana.Lakini watu hawaoni hayo." kilio cha walimu ni kurudishiwa Teaching allowance".

No comments:

Post a Comment