Saturday, July 7, 2012

WAZIRI MKUU MHE,MIZENGO PINDA AZINDUA NA KUGAWA MATREKTA 33 KATI YA 53 YANAYOKOPESHWA KWA WAKULIMA WA MKOA WA RUVUMA,KUONDOKANA NA JEMBE LA MKONO

 Waziri Mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Mizengo Pinda leo amezindua mradi wa matrekta 53 na kati ya hayo 33 yameshapata wanunuzi ambao wamekabidhiwa fungu na Mhe Waziri Mkuu katika viwanja vya Zimani Moto Songea leo.
Baada ya kukata utepe Waziri Mkuu alijaribu kuliwasha trekta lililokopwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe.Said Thabit Mwambungu.
Aidha alisema matrekta hayo lazima yapelekwe shambani,si vinginevyo,na kwamba amewataka Halmashauri zote nchini kupunguza utitiri wa vikwazo vya mazo katika barabara.
Waziri Mkuu alikuwa akiwaonyesha watu namna trekta linavyo weza kuwa msaada na ukombozi mkubwa kwa mkulima.

No comments:

Post a Comment