Sunday, July 8, 2012

CHUO KIKUU CHA SAUT SONGEA KUANZISHA EVINING CLASS KUANZIA MWEZI WA 9 MWAKA HUU

               CHUO KIKUU CHA SAUT SONGEA KUONGEZA VITIVO

MSHAURI wa wanachuo ( Dean of Student ) Michael Sinienga alisema hayo hivi karibuni kwa waandhishi wa habari wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wa Kanda ya Kusini walipotembelea chuo hicho kwa lengo la kupata taarifa za mafanikio na changamoto kadhaa tangu chuo hicho kianze kudahili wanachuo wake.
     Bwana Sinienga alitaja vitivo vitakavyo ongezeka kuwa ni pamoja na ‘Business Administration, Law, Medicine, Mass Communication  and Education’ ambayo ndiyo iliyoanza.
   Matarajio mengine ya chuo hicho ni kutoa kozi fupifupi za ujasiliamali, kozi za jioni ‘Evening classes’  kwa watumishi na watu wengine wenye kutaka kusomea shahada wakiwa kazini.
    Matarajio mengine ni kutoa huduma kwa shule za sekondari ambazo zitakuwa na uhaba walimu na zikipenda kupata huduma hiyo kutoka katika Chuo Kikuu hicho, Pia kuwaandaa vijana kujiamini na kujitambua na maadili kuwekewa kipaumbele.






1 comment:

  1. Nilipata fursa, juzi Jumamosi, ya kutembelea chuo hiki kipya. Alinitembeza mwenye kigoda wa chuo, Profesa Donatus Komba, akanieleza mengi kuhusu historia, mipango, na changamoto za chuo hiki. Niliondoka nikiwa nimefahamu mengi na pia nikiwa na ari ya kuchangia juhudi za hao wenzangu.

    ReplyDelete