Saturday, July 21, 2012

WAFANYA BIASHARA WASISABISHE MWEZI RAMADHANI KUWA MWEZI WA MAJONZI NA MAJUTO BADALA YA FARAJA KWA WANAO FUNGA -SHEKHE JONGO

Shekhe Himidi Jongo akielezea umuhimu wa mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ambapo leo ni mfungo mosi.Aidha na kuwaomba wafanya biashara nchini kuacha kupandisha bidhaa bei.


Wafanya biashara wameshauriwa kuacha kupandisha vitu bei kwa sababu ya mfungo wa Ramadhani,Shekhe Hamidi Jongo wa Dar es Salaam alisema hayo kwenye kipindi maalumu cha TBC jana wakati akielezea umuhimu wa kufunga kwa waumini wa Dini ya Kiislam.
Alisema Mungu alihalalisha biashara kufanyika na aliharamisha riba katika biashara,hivyo kufanya bishara siyo dhambi  bali kupandisha vyakula wakati huu wa mwezi Mtukufu wa ramadhani ni dhambi kwani bei ya jana kabla ya mfungo kwa nazi,mhogo,mchele kwanini leo siku ya mfungo mosi ipande? ‘Wasifanye mwezi Ramadhani uwe ni mwezi wa Majonzi na majuto badala ya faraja kwa wanaofunga’ alisema Shekhe Jongo.
Aidha alisema kwa mfanya biashara wa Kiislamu awe mkweli kwa wateja wake wakifika kununua mchele au maharage asema kweli kuwa maharage yake yanaiva haraka au yanachelewa kuliko kusema maharage yake ni maji mara moja kumbe uongo.Mtu kama huyo asifunge maana atakuwa anapoteza muda wake bure.
Tuungane na Shekhe  Jongo kuwahasa wafanya biashara wa mhogo,maharage,nazi,tambi,tende wauze bidhaa hizo kwa bei ya halali,wasipandishe bidha hizo muhimu kwani kufanya hivyo ni kuwakomoa  wenzetu watakaojaliwa kufunga,kwani mwezi huu ni mwezi  Mtukufu kwa waumini wa Kiislamu.

1 comment:

  1. Kila unapofika Mwezi Mtukufu, tunasikia taarifa za huu ufisadi wa kupandisha bei. Sijui kama hao mafisadi ni wa dini gani au labda ni makafiri. Ingekuwa bora kama kungekuwa na utaratibu wa kuwataja, ili ijulikane hao wahujumu wa dini ni akina nani.

    ReplyDelete