Saturday, July 14, 2012

WANANCHI KUTOA USHIRIKIANO KWA MAKARANI WA SENSA SIKU YA TAREHE 25 /8/2012 SIKU YA KUHESABIWA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Mizengo Pinda alisema kuwa siku ya tarehe 25 mwezi wa nane mwaka huu makarani wa sensa watapita katika kaya za watu kuhesabu,kuelewa siku ya kuamkia tarehe 25 ni watu wangapi wamelala katika nyumba ile.
Aidha Mhe.Pinda alisema kuwa wananchi wajitokeze kutoa maoni yao kuhusu Katiba mpya siku Tume ya Katiba ikifika katika maeneo yao.
Mhe.Pinda alisema hayo siku akizindua mradi wa matrekta katika uwanja wa Zimani moto katika Manispaa ya Songea hivi karibuni,siku ya pili ya ziara yake ya siku mbili ya kikazi Mkoani Ruvuma.

No comments:

Post a Comment