Friday, May 3, 2013

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII ASEMA OPERESHINI YA KUPAMBANA NA MAJANGILI WA WANYAMA PORI LAZIMA IFANYIKE, JANA BUNGENI DODOMA

 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi Kagasheki,alisema kuwa operesheni ya kupambana na majangiri wanao vamia hifedhi na kuu wanyama bila kuwa na kibali  Serikali itafanya peresheni hiyo kwa kusitukiza.Balozi Kagasheli alisema hayo wakati akijibu hoja mbalimbali za waheshimiwa Wabunge katika ukumbi wa Bunge mjini Dodoma jana.
Katika mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo,Mhe. Kagasheki alisema tatizo la ujangiri wa wanyama pori sio la Tanzania peke yake,bali ni kilio cha nchi nyingi zenye Game Reserve na National Parks ,alisema ujangiri umekuwa wa hali ya juu kwa sababu ya mahitaji ya pembe za ndovu na kifaru katika soko la dunia.

No comments:

Post a Comment