Thursday, May 16, 2013

ASKOFU MKUU WA JIMBO KUU LA SONGEA MHASHAMU NOBERT MTEGA, AKUBALIWA OMBI LAKE LA KUSTAAFU KUTOKANA AFYA YAKE KUTOKA KWA BABA MTAKATIFU FRANCIS , VATCAN CITY ROMA, NAWALA HAJAJIUZURU KAMA ILIVYO TANGAZWA NA BAADHI YA VYOMBO VYA HABARI

 Askofu Mstaafu Norbet Mtega akihojiwa na Vyombo vya habari kuhusu uamuzi wa Kustaafu kazi za utume wake kabla ya miaka 75 ambayo Askofu anatakiwa kuomba kustaafu.
 Mahojiano na waandishi wa habari
 Picha ya pamoja na waandishi wa habari katika Bustani ya nyumba ya Uaskofuni Mjini Songea leo.
 Picha ya pamoja
 Picha ya pamoja na  Mhashamu Askofu Mtega
 Askofu Mtega akiwa na mtangazaji wa Radio Maria Mbinga Bw. Nilai  wa kushoto na Mwandishi wa habari mpiga picha Bw. Ndolanga na Nyuma yake Askofu ni Bibi Joyce Joliga mwandishi wa habari Gazeti la Mwananchi
Ni picha ya Pamoja ya Mwandishi wa habari wa TBC Bw.Gerson Msigwa na Askofu Mtega



Kauli hiyo ameitoa leo mbele ya vyombo vya habari alipokuwa akiongea navyo katika bustani ya nyumba ya uaskofuni katika kanisa kuu la Mtakatifu Mathias Mulumba Kalemba la Mjini Songea.
Askofu Mtega alisema ni vyema kuacha mapema kazi wakati mtu akiwa na nguvu,akili kuliko kusubili mpaka akili ichoke kwa kusahau mambo.
Alisema ameomba kustaafu kabla ya miaka ya kustaafu kwa maaskofu wa miaka 75.kutokana na matatizo ya kiafya ,mara nyingine anasumbuliwa  na BP.
Askofu Mtega amefanya utume wake kwa miaka 28 ambapo Mkoani Iringa ametumikia kwa miaka 6 na Jimbo Kuu la Songea ametumikia miaka 22, na kutoa huduma za kiroho na za kijamii zikiwemo za Elimu ,Afya pamoja na Mazingira.
Amesema kuwa yeye bado ni Askofu na atafanya kazi zote atakazo ambiwa kufanya na Askofu Mkuu atakayeteuliwa, ambapo kwa sasa anashikilia Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Mhashamu Ngalalimnamtwa wa Iringa.
Amewashukuru waumini wote kwa ushirikiano mwema waliouonyesha wakati wa utume wake,na  amekuwa nao kwa moyo mmoja bila kukwaruzana wala kugombana, aidha ameomba ushirikiani uimarike na kufanya kazi bila kuingiza ukabila maana masuala ya ukabila yilipitwa na wakati.

No comments:

Post a Comment