Wednesday, March 7, 2012

SONGEA SASA SHWARI,ULINZI WA SUNGUSUNGU UMESHAMIRI AMANI NA UTULIVI VIMETAWALA

Agizo la Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mhe.Said Thabit Mwambungu la kuwa taka wananchi wa Manispaa ya Songea kushirikiana na Jeshi la polisi katika kuiweka Manispaa hiyo katika hali ya utulivu kwa wananchi wanaoishi katika Manispaa hiyo limefanikiwa kwani wananchi wanafanya shughuli zao na wanalala kwa amni..
Mhe. Mwambungu alitoa agizo hilo katika kikao kilichoitishwa na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya na Mkoa wakati wa wimbi la mauaji lilivyo ibuka katika Manispaa hiyo mwezi uliyopita ,na kusababisha wananchi kuandamana na kusababisha vurugu zilizo ondoa amani.
Hali ya utulivu imerejea kama awali,wananchi kupitia viongozi wao wa mitaa wanalinda katika mitaa yao,kuhakikisha usalama unakuwepo,wakitumia ulinzi shirikishi ( sungusungu ) kuna kila dalili ya kumpongeza mkuu huyo wa mkoa na uongozi wote wa wilaya na mkoa kwa pamoja kwa uamuzi walio uchukua.

No comments:

Post a Comment