Thursday, March 8, 2012

SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO, NI SIKU MUHIMU SANA KWANI MWALIMU WA KWANZA KATIKA FAMILIA NI MWANAMKE KISHA NI MAMA KATIKA JAMII DUNIANI NANI KAMA MAMA

 Wanawake wa mkoa wa Ruvuma leo wameungana na wanawake wezao Duniani kuadhimisha siku yao leo ambayo kila mwaka inaadhimishwa Duniani,na kwamba Ushirikishwaji  wa wasichana katika maendeleo ni chachu ya  maendeleo.Wanawake hao wa mkoa wa Ruvuma  wanasema kuwa wao hawafungamani na chama chochote.
 Ni baadhi ya wanawake wakiwa katika makumbusho ya majimaji  mjini Songea siku ya kupinga ukatili wa kijinsia ,iliyofanyika mwaka jana.
Aidha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe.Said Thabit Mwambungu wamewaambia wanawake wa mkoa wa Ruvuma leo kushikamana katika vikundi vya uzalishaji mali na kujiunga katika SACCOS ili wasiwe tegemezi zaidi kutoka kwa wanaume katika Wilaya Mbinga Kijiji cha Mkako ambapo leo alikuwa mgeni rasmi.

No comments:

Post a Comment