Saturday, March 10, 2012

KAMATI YA KUCHUNGUZA VURUGU ZILIZOTOKEA TAREHE 22 FEBRUARI 2012 ILIYOUNDWA NA MKUU WA MKOA IMETOA TAARIFA YAKE RASMI JANA

 Mheshimiwa Mkuu  Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu akitoa taarifa ya kamati aliyoiunda kuchunguza vurugu zilizotokea tarehe 22 mwezi Februaru mwaka huu katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma kwa waandishiwa wa habari jana ofisini kwake.
 Baadhi ya waandishi wa habari nikiwemo pamoja nao tukifuatilia taarifa hiyo hapo jana ya mkuu wa mkoa wa Ruvuma.
baadhi ya viongozi wa mkoa na Mkuu wa wilaya ya Songea Ole Thomas Sabaya na waandishi wa habari katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Ruvuma wakisikilizataarifa ya kamati hiyo.


KAMATI iliyoiundwa kwa mazumuni ya kuangalia vurugu zilizotokea na kuleta mataizo makubwa,  tarehe 22 februari mwaka huu na kupelekea watu watatu walipoteza maisha yao wakiwemo wawili kwa kupigwa na risasi na mwingine kwa ajali ya pikipiki na wengine kadhaa kupata majeraha ambao walipata matibabu na halizao zikawa  salama.Mkuu wa mkoa Mhe.Said Thabit Mwambungu amaipokea taarifa yao.

Mkuu wa mkoa huyo aliunda  Kamati  ya watu 8 iliyoongozwa na Katibu Tawala msaidi wa mkoa  nayeshughulikia miundombinu Injinia Tossi na wenzake maafisa waandamizi  7 kuangalia chanzo cha vurugu ile kama ilikuwa vipi ili isije jirudia tena.

Alisema nia ya serikali ni kusalifu kiundani chanzo cha vurugu ile ili serikali ifanye kazi yake na pia wananchi waelewe kuwa serikali imepokea taarifa ile,na kubaini mambo kadhaa, yakiwemo ya  kiutawala   na  ya kisheria.

Ambapo mengine yameanza fanyiwa kazi kwa mujibu wa sheria.kwa kuwafikisha kunako husika watuhumiwa waliyohusika na mauaji toka Mwezi Novema mwaka jana Na kesi zao zipo katika hatua mbalimbali.

Alisema na wale ambao walihusika na mauaji ya vijana wawili kwa risasi watafikishwa kwenye vyombo vya sheria lili uchunguzi ufanyike na haki itendeke kwa mujibu wa sheria.

Aliwaomba wananchi waepukane kueneza  uvumi ambao unaweza kuzalisha maafa makubwa katika jamii na wanaposikia jambo au tetesi ya uhalifu wapeleke taarifa kunako husika. kuliko kuchukua sheria mikononi.

Alisema wananchi wamepata elimu ya kujilinda na kazi hiyo imeanza kwa ulinzi shirikishi katika mitaa yote ya Mansipaa ya Songea.Baada ya wananchi kuelewa umuhimu wa kujilinda,.na kuwa na tabia ya kufikisha malalamiko yao kunako husika kwa njia ya halali  na ya amani kwenye vyombo vya sheria.  Na kwamba sungusungu wametakiwa kufanya kazi yao kwa kufuata sheria na wanapompata mhalifu wasichukue sheria mikononi wamfikishe kwenye usalama.

Pia Mhe.Mwambungu aliwashukuru wananchi na waandishi wa habari kwa ushirikiano wao na serikali katika kuifanya manispaa ya songea kurejea katika hali ya usalama na utulivu kwa muda mfupi sana.

Aidha aliwataka wananchi wa nje ya mkoa huo kuwa hali ya utulivu na amani katika mkoa wa Ruvuma na wilaya zake zipo kama mwanzo, ambapo wananchi wanafanya kazi zao kama kawaida za kilimo na zauzalishaji mali.

                                                                                                                                

No comments:

Post a Comment