Tuesday, October 6, 2015

WAKATI ZIMEBAKI SIKU CHAHCE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA MADIWANI,WAGUNGE NA URAIS,WATANZANIA WAMETAKIWA KUWA KUTUNZA SHAHADA ZAO ZAKUPIGIA KURA

Baadhi ya wananchi wenye kuipenda amani utulivu,pamoja na utulivu, upendo kwa atanzania wote kuacha kuwahadaa watu  wenye shahada zao za kupigia kura kuzifanya ziwe bidhaa kwa mafaniko yao katika kuchaguzi ujao.

 Aidha wanaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kusikiliza Sera za wagombea mbalimbali wa vyama vyote ,ili wajue na wachambue mbivu na mbicha tarehe 25 mwezi huu.

Lakini sanasana cha muhimu ni kuaandaa mazingira ya Amani ,utulivu siku hiyo ya kupiga kura.Hasa kila mmoja amalizapo kufanya kitendo cha haki yake ya kumchagua Diwani,Mbunge na Rais tarehe 25, arudi nyumbani kwakwe kusubili matokeo.

Wale ambao wanatarajia kubakia vituoni kusubiri kuona aliyemchagua kashinda,waache kwani kufanya hivyo kutasababisha uvunjifu wa Amani.Nini maada ya mawakala wa vyama na Tume ya Uchaguzi,Kazi ya kutangaza matokeo ni Tume ya Uchaguzi wengine Turudi majumbani mwetu.

Inajulikana kuwa kura ni siri ya mpiga kura,sasa wewe mwingine kushabikia fulani lazima ashinde je wewe ulikuwa na wapigakura wote nchini ukaona wamemchagua huyo unaye sisitita kuwa kashinda ,jamani tuwaachie wenyewe watakao hesabu kura na kutoa matangazo.

Blogu hii imesikiliza maoni ya baadhi ya Wananchi wa Dodoma wakielezea mtazamo wao katika mwelekeo wa Uchaguzi mkuu tarehe 25 mwezi huu,na kwamba iwapo wananchi watafuata maelekezo ya Tume ya Uchaguzi na Vyombo vya Ulinzi na Usalama ,Uchaguzi siku hiyo utakuwa wa  Amani na Utulivu kwani Tanzania ni Kisiwa cha Amani.Hivyo tumuombe Mungu aifanye siku hiyo iwe ya Amani na Utulivu na Atuongoze katika kuwapata viongozi ambao ni chaguo lake.

No comments:

Post a Comment