Monday, October 26, 2015

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YATANGAZA MATOKEO YA URAIS KUPITIA VYOMBO VYA HABARI ,NA KUTOA ANGALIZO

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva ameanza kutangaza matokeo ya Urais ambapo Kupitia CCM Dr. Joseph Pombe Magufuli anaonekana kuongoza akifuatiwa na wa CHADEMA Edward Lowassa.Jaji Lubuva amewaambia wandishi wa habari kuwa  kesho saa tatu asubuhi. ataendelea kutangza matokeo mengine yatakayo pokelewa kutoka  kwenye Majimbo ya uchaguzi nchini.

Aidha alisema kuwa mwenye mamlaka ya kutangaza matokeo ya Urai ni Tume ya Uchaguzi ya Taifa peke yake, mtu mwingine atakapo tangaza yatakuwa siyo matokeo rasmi.Na kwamba aliwaonyesha waandishi wa habari makaratasi yaliyo sainiwa na mawakala wa vyama vyao.na kutumwa Tume ili yatangazwe.

No comments:

Post a Comment