Saturday, October 24, 2015

KITUO CHA KUPIGIA KURA CHA OFISI ZA SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA DODOMA SAA MOJA KAMILI WANANCHI WALIANZA KUPIGA KURA,KWA AMANI NA UTULIVU MKUBWA

  • Kuona jinsi wananchi walivyo hamasika wengi wamejitokeza kwa wingi kwenda kutimiza haki zao za msingi  cha chagua viongozi wanao wataka.
  • Mabasi yakutoka na kuingia kwenye stendi ya mabasi Mkoa wa Dodoma  hayapo wasafiri nao hawapo stendi imetulia kama vile watu hawapo.
  • Kwenye Zahanati ya Mkole nako hata wagonjwa nao hawapo pametulia.
  • Barabara na mitaa ya Mji wa Dodoma kumetulia .ukweli hali ni shwari.
  • Kituo hicho hali nishwari kabisa ,wanamama,wazee,na vijana wamejitokeza na wameelekezwa vya kutosha.

 Foleni ya wapiga kura katika kituo cha ofisi za Shirika la Nyumba na Taifa wakiwa katika kusubiri zamu zao  za kupiga kura zifike
  • Hii barabara ya kutoka Bungeni kuelekea mjini iko tupu
Foleni ya wapiga kura pamoja wa waandishi wa habari wako sambamba kufuatilia mwenendo mzima wa kupiga kura,akiwemo wa ITV na vymombo vingine li kuhabarisha Taifa na Dunia kwa ujumla kuonyesha jinsi Tanzania ilivyo kuwa na Ukomavu wa Vyama vingi na kuzingatia Democrasia ya kweli..


Hiki ni kituo cha Zahanati cha Makole kumekuwa na utulivu kama vile wagonjwa hawapo,lakini yote ni kwenda kupiga kura.

No comments:

Post a Comment