Wednesday, October 21, 2015

WAKATI ZIMEBAKIA SIKU TATU WATANZANIA WATUMIE HAKI YAO YA KUCHAGUA VIONGOZI WANAO WATAKA MKURUGENZI WA HUDUMA ZA SHERIA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI BWANA EMANNUEL KAVISHE ASEMA MWENYE KUTANGAZA MATOKEO NI TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

Aidha Bw. Kavishe amesema Viongozi wa Vyama na wananchi wanatakiwa kupiga kura zao kwa amani na utulivu na kwamba ,baada ya kupiga kura watu warudi walikotoka na kusubili matokeo ambayo yatangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Amesema Mtu atayepata kura nyingi atatangazwa kutoka kwenye chama chochote ambacho mgombea amepata kura nyingi.
kuhusu idadi kamili ya wapiga kura tarehe 25 mwezi huu ,amesema kuwa ni watu milioni 22..7 ambao wanatarajiwa katika upigaji kura siku hiyo,nakwamba kila mtu atapiga  kura kwenye kituo alichojiandikisha,na kama yuko nje ya kituo chake basi mtu huyo atakuwa amekosa haki yake ya kumchagua kiongozi anaye mtaka.
Pia kasema ili kuepusha vurugu zisizo na sababu wananchi wafuate maelekezo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi,na kuheshimu Katiba.Na madai ya kubaki kwenye vituo baada ya kupiga kura, inamaana mawakala waliyowekwa na vyama vyao hawaviamini.maana waele ndiyo watao hakikisha mgombea wake amepata kura ngapi.

No comments:

Post a Comment