Wednesday, June 17, 2015

NG,OMBE 94 NA MBUZI 75 WA MFUGAJI MMOJA JINA LAKE HALIJAPATIKANA KATIKA MANISPAA YA DODOMA WAMESHIKWA WAKIWA SAZURULA KATIKA MANISPAA HIYO KUTOKANA NA KUKIUKA AGIZO LA SERIKALI LA KUHAMISHA MIFUGO YOTE KWENDA NJE YA MANISPAA

Uongozi wa Manispaa ya Dodoma ilishatoa agizo kuwa kila mfugaji ahamishe mifugo yake kupeleke nje ya Manispaa,na atakayekiuka agizo hilo ng,ombe akikamatwa atapaswa kumlipia shilingi 20,000 na mbuzi shilingi 10,000.kila mmoja.
Kwa hiyo mfugaji huyo anang,ombe 94 kila mmoja shilingi 20,000 sawa na shilingi 1,880,000 na mbuzi 75 ikiwamo mmoja shilingi 10,000 ,mfugaji huyo italazimu kulipa shilingi 2,630,000 kwa sababu ya kiburi na ujeuri wa kupingana na maagizo yanayotolewa na Serikali.
Mmoja anayeshughulikia mifugo inayo zurula hovyo katika Manispaa hii alisema,mara nyingi wenye mifugo wamelekezwa nini cha kufanya,lakini wanakiuka,nakwamba mjini kuwepo na mifugo inayochungwa haileti picha nzuri ni vyema watoe ushirikiano na mamlaka husika ,kuhamisha mifugo mbali na Mji.

No comments:

Post a Comment