Wednesday, June 17, 2015

JAJI MKUU MSTAAFU AGUSTINO STIVIN RAURENCE RAMADHANI ASEMA ANAUWEZO WA KUWA RAIS IWAPO CHAMA CHAKE KITAMPA RIDHAA YA KUONGOZA


Jaji Ramadhani aliwahikuwa askari kwa cheo cha Luteni Usu mwaka 1971 na hatimaye Brigedia Jenerali,vita vya Uganda naye alikuwemo.akaongeza kuwa mwaka 1978 alikuwa Naibu Katibu Mkuu Zanzibar.


Alisema kuwa baadaye aliteuliwa kuwa Jaji Mkuu Zanzibar na hatimaye Tanzania Bara hadi kustafu kwake,na kwamba hadi sasa ni Jaji Mkuu wa Afrika na ni Mtanzania wa kwanza kushika nafasi hiyo, hivyo kutokana nafasi yake aliyokuwa nayo anasema anauzoefu na anauwezo na sifa za kuwa Rais wa Nchi hii.Pia ni msafi hana tuhuma za rushwa.

Kuhusu mauaji ya wenye ulemavu wa ngozi ,amesema yeye akiwa Rais atahakikisha kunatolewa elimu kwa wananchi kuondoa imani potofu ya kuwa viungo vya Albino vinampa mtu utajiri au cheo nasio mwili mzima.na kwamba serikali iliyoko madarakani imeshaanza kuchukua hatua kali kwa wale waliobainika wamefanya mauaji kwa walemavu wa ngozi hao.

Aidha akiwajibu waandishi wa habari kuhusu kuwa na wafuasi wengi wakati wa kuchukua fomu, alisema .sipendi makeke wakati wa kuchukua fomu,asema kibaya chajitembeza na kizuri chajiuza.

Jaji Ramadhan amekabidhiwa fomu kadhaa zikiwemo za kupeleka mikoani kuomba wadhamini,na kisha kuzirudisha kwenye ofisi za Chama hicho Mjini hapa.

No comments:

Post a Comment