Friday, September 12, 2014

MWENYEKITI WA TCD MHE. MOMOSE CHEYO ASEMA RAIS JAKAYA KIKWETE ALIKUTANA NA TCD NA SIYO ALIKUTANA NA UKAWA MJINI DODOMA

Hayo yalisemwa na mwenyekiti huyo kwenye kipindi cha Jambo kinachorushwa na TBC1 kuwa hakupenda vichwa vya baadhi ya magazeti kuandika " Kikwete akutana na UKAWA Mjini Dodoma" bali ilitakiwa iwe Kikwete akutana na TCD Mjini Dodoma.

Aidha alisema kuwa mazungumzo yao na Rais yakifikia makubaliano,lakini cha ajabu bado kuna baadhi yao wamekuwa wagumu kurudi Bungeni kuendelea na majadiliano ya Rasim ya Katiba.

Alisema Bunge maalumu la Katiba lipo kisheria hivyo haliwezi kuvunjwa kwa ajili ya watu wachache walioko nje ya Bunge, bali litaendelea hadi tarehe 4/10/2014.na kwamba amewasihi wananchi kuwa waulivu kazi waliyo watuma inaendelea vizuri.

Na hakuna chama kinacho taka nchi iingie kwenye vurugu,aidha vijana wasichochewe na wachache hao kwa madai ya kuingia barabarani,kwani watakao pata madhara wao wenyewe watakuwa mbali hiyo ndiyo sifa ya wachochezi.

No comments:

Post a Comment