Monday, July 15, 2013

WAZIRI MKUU WA JAMHURU YA MUUNGANO WA TANZANIA MIZENGO KAYANZA PINDA AWEKA JIWE LA MSINGI LA CHUO CHA UALIMU KIUMA BONITE TUNDURU

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Mizengo Kayanza Pinda


WARIZRI Mkuu Mhe. Mizengo Kayanza Pinda ameweka jiwe la msingi chuo cha Ualimu Kiuma Bonite Tunduru ,Chuo  kinacho milikiwa na Mkurugenzi Dkt.Matomola,ikiwa ni Taasisi kubwa inayo unganisha Chuo cha Waganga,shule msingi na  sekondari na shughuli nyingine za maendeleo.
Mhe.Pinda alisema kuwa Serikali inatambua mchango wa shirika hilo la Bonite ambalo linaliletea maendeli wananchi wa Tunduru, Mkoa wa Ruvuma na majirani pamoja na Taifa kwa ujumla.na kwamba alimshukuru sana Dkt Matomola kwa moyo wake wa uzalendo wa kuanzisha taasisi kubwa kama ile kwa manufaa ya taifa, badala ya kujinufaisha mwenyewe.
Aidha mhe.Pinda katika mkutano na  wananchi mjini Tunduru leo, alisema ushururu kwa watu wadogo wadogo usitozwe, maana unaleta kero kwa wananchi wa hali ya chini.
Kuhusu maendeleo ya elimu wilayani humo, Mhe. Pinda amemwambia Mkuu wa mkoa kuwa asili 30 ya watoto wote waliyo faulu kuingia Kidato cha kwanza, ambao hawaja ripoti waende shule mara moja.
Ambapo kuhusu ujenzi kwa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Namtumbo hadi Tunduru utaendelea kujengwa baada ya wakandarasi wa  awali kufukuzwa kwa kushinda kukamilisha katika muda waliyo pangiwa.
Waziri Mkuu amesikia kilio cha watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ambao wamekaa  kwa miaka mingi bila kupata uhamisho kama vile ndiyo wamehamia, amewaambia mara baada ya kufika Songea ataangalia nini cha kufanya. ( Na. Juma Nyumayo katika Msafara wa Waziri Mkuu mkoani Ruvuma )

No comments:

Post a Comment