Tuesday, September 11, 2012

MAANDAMANO YA AMANI YA WAANDISHI WA HABARI NCHINI ,KAGERA WAMTAKA KAMUHANDA KAMANDA WA IRINGA KUJIUZURU

 Maandamano ya waandishi wa habari ya amani kufuatia kifo cha mwandishi mwenzao wa Channel Ten na mwenyekiti wa Iringa Press Club David Mwangosi aliye uliwa na Jeshi la Polisi Mkoani humi mbele ya kamanda wa Polisi wa mkoa huo Michael Kamuhanda.Wandishi wa habari wa mkoa wa Kagera wanitaka serikali kumwajibisha kanda huyo,na nafasi yake akaimishwa RTO wakati taratibu za kishria zikifanyika.
 Nako mkoani Kilimanjaro waandishi wanalaani vikali mauaji ya kinyama yaliyofanyika Mkoani Iringa ya mwandishi mwenzao,wanasema askari wanakiuka viapo walivyo apa wakiwa katika mafunzo yao kuwa watalinda raia na mali zao,badala yake wanaua raia.wameomba serikali kufuatila mauaji hayo.
Dar es Salaam wandishi uzalendo uliwashinda pale waziri mwenye dhamana alipo taka kwenda kuwasikiliza kumkataa na kutimua kwa kuwa hakuhusika.Dr.Emanuel Nchimbi.wakati amevalia suti nyeupe kwenye msiba wa wanahabari hao,wengine waliwaponda askari kwa maneno makali.
 Lakini je Jeshi la polisi kwa nini wanatumia silaha kubwa kubwa kutuliza ghasia? hivyo bom lililotumika kumlipulia mwandishi huyo ,ilikuwa ni mahali pake? isitoshe mwandishi anasulubiwa na kutekezwa mbele ya Kamanda wa polisi wa mkoa bila ya kukemea,au jeshi hilo mkoani humo walikuwa wanamtafutia kosa la kummaliza.Wanahabari na kalamu zao waliuliza Jeshi la polisi linamchukuliaje kamanda wa polisi wa mkoa huo na muuwaji wake.Familia ya marehemu Mwangosi serikali itawatunza? au la.
Wananchi na waandishi wa habari watashindwa kufanya kazi zao kwa kuwaogopa polisi,Inatisha kusikia kuwa Mwanshi wa Iringa ndiye iliyetoa siri ya askari polisi wetu kwa mauaji ya waandishi wa habari kisirisiri,wapatao 46.Kama ilikuwa ni kutuliza maandamano ya Chama kwanini Bomu hilo wange walipua viongozi wa chama chenyewe,na badala yake kumua mwandishi inasikitisha.Ukweli IGP asema kitu kwa waandishi kuhusu hatima ya matumizi nguvu kubwa katika kutuliza ghasia nchini na viongozi wazembe katika Jeshi lake.Mungu aiweke Roho ya Marehemu Mwangosi mahali pema peponi Amin.

No comments:

Post a Comment