Sunday, August 26, 2012

RAIS AHESABIWA NA FAMILIA YAKE NYUMBANI KWAKE IKULU,KISHA KUZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI NA KUSEMA WAACHE KUANDIKA HABARI ZA KUCHOCHEA

 Rais Kikwete azungumza na waandishi wa habari leo Ikulu baada ya kuhesabiwa na familia yake
 Kikwete akisikilia maswali kutoka kwa waandishi wa habari Ikulu Jijini Dar es Salaam leo baada ya kuhesabiwa
 Rais akiwaambia waandishi hao kuacha kuandika habari za uchochezi zitakazo wafanya waliyojifungia msikitini kuwa na nguvu zaidi.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akipigilia msumari kwa wale waliyo patikana na nyaraka za kuwaasa waislamu wasihesabiwe akiwemo kijana wa Chuo kikuu,alisema ndani yake wapo viongozi wakubwa na wanatambulika kwa majina ila hakuna haja ya kuwatangaza kupitia vyombo vya habari .' Hao tutakula nao ' alisema.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete amehesabiwa na familia yake nyumbani kwake Ikulu leo asubuhi,katika chumba cha siri kwakuwa sensa ni siri ya anae hesabiwa na karani wa sensa.
Baada ya kuhesabiwa Rais aliongea na waandishi wa habari waliyofika katika zoezi hilo,ambapo alirudia yale ambayo aliyazungumza katika hotuba yake aliyoitoa kupitia vyombo vya habari.
Aidha waandishi nao waliuliza kuwa baadhi ya watu wameonekana kuwa wamefanya vitendo vya kushawishi watu wasihesabiwe kwanini wasichukuliwe hatua za kisheria.Rais aliwajibu kuwa maelekezo yametolewa jana kupitia hotuba yake na kwamba kwa kua zoezi ni la siku 7 watu hao watashughulikiwa iwapo watazidi kuendelea na harakati zao.
Ila alitoa angalizo kwa vyombo vya habari kuandika habari za kuchochea,maana habari mbaya kwao ndiyo habari nzuri.wakizisikia wanajua kuwa hoja zao zimesikika,hasa wale waliyo jifungia katika misikiti Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment