Sunday, August 26, 2012

Mjusi na takwimu za mashirika isiwe sababu ya kususia Sensa – Dr.Kikwete

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aongea na wananchi kupitia vyombo vya habari ,kama kaida yake kwa lengo la kusisitiza umuhimu wa kuhesabiwa katika Sensa iliyoanza saa 6 usiku kwa wasafiri na wenye mazingira magumu.





RAIS wa Jamhuri ya Tanzania Dr.Jakaya Kikwete amewaasa wananchi kujitokeza katika sensa iliyoanza jana usiku  kwa wasafiri na watu walioko katika mazingira magumu,kuhesabiwa na kuwapa ushirikiano wa kutosha Makarani wa Sena,na kwamba madai ya kurudishwa mifupa ya Mjunsi iliyoko Ujerumani,na madai ya viongozi na wanaharakati wa Dini ya kiislamu ya Takwimu zilizotolewa na mashirika visiwe vigezo vya kususia Sensa.
Alisema kuwa kususia sensa kwa sababu hizo ni kutoitendea haki serikali,kwa kuwa taarifa za Takwimu zinatolewa na ofisi ya Taifa ya Sensa na siyo ya mashirika.na katika sensa hakuna masuala ya udini au rangi,Sera yetu haiusiki na sera za ubaguzi wa rangi au udini kama ilivyo wakati wa Ukoloni,kwa kuwa wakoloni walikuwa na Sera za ubaguzi.
    Hivyo Rais amewataka wananchi kushiriki katika Sensa kwa maendeleo ya Taifa letu na si vingine,Aidha amewataka viongozi wa vyama,Serikali kusimamia zoezi hili lifanikiwe katika maeneo yao.
      Katika Mkoa wa Ruvuma zoezi hilo limeanza ,ambapo makarani wa Sensa wameshapata vifaa vyote vinavyo husiana na zoezi hili na hivi sapo katika kuhesabu watu katika kata zao.Ikiwemo Mtaa wa Sabasaba na nje ya uwanja wa sabasaba Matarawe manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.Katani wa Sensa Bi. Maria Kibumu na Mjumbe wake  Razalo Luambano wamesha pitia zaidi ya kaya 5 na wanasema hawaja kumbana na matatizo yoyote hadi muda tuna kwenda mitamboni.



No comments:

Post a Comment